Watu 63 wapoteza maisha Hanangi, zaidi ya 100 wajeruhiwa

 

Takribani watu 63 wamepoteza maisha na wengine zaidi ya 90 kujeruhiwa kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo katika eneo la Katesh wilayani Hanang mkoani Manyara nchini Tanzania.

 

Tukio hili la kutisha limetokea jana jumapili kufuatia mvua nyingi zinazoendelea kunyesha katika maeneoo mbalimbali nchini humo ambapo inaelezwa kuwa mamia ya makazi yameharibiwa, na watu kukosa sehemu za kujistili na miundo mbinu mingi kuharibika ikiwemo Barabara katika kanda ya kaskazini hususani mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, na Manyara.

 

Waliojeruhiwa wamekuwa wakipatiwa huduma mbalimbali za kibinadamu ikiwemo matibabu na kuruhusiwa hali zao zinapokuwa zimeimarika na wengine wamekuwa wakipelekwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu Zaidi kwa waliojeruhiwa vibaya.

 

Taarifa zinasema kuwa chanzo cha janga hiyo kwa mkoa wa Manyara ni mvua nyingi zilizopelekea kuporomoka kwa sehemu ya Mlima Hanang ulioko Jirani na mji wa Kateshi ambao sehemu yake kubwa imekubwa na athari zinazotokana na mafuriko ya tope, maporomoko yam awe na maji mengi katika makazi ya watu na vituo vya huduma za umma.

 

Akizungumza na wanahabari, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga amesema eneo kubwa lililoathirika na mafuriko hayo ni kata ya Gendabi katikati ya mji wa Katesh.


Mh. Queen Sendiga (mwenye fulana nyekundu) akiongoza kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa manyara katika kushughulikia changamoto mbalimbali kufuatia mafuriko na maporomoko ya udongo Kateshi


Kikosi cha kupambana na maafa chini ya Ofisi ya Waziri mkuu kimetumwa Katesh kufanya shughuli mbalimbali za uokoaji ambapo tayari kambi tatu zimeandaliwa kwa ajili ya kuwapatia hifadhi watu waliokosa kabisa mahali pa kuishi.

 

Kufuatia janga hilo Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan ambaye yuko Dubai kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa mazingira COP, ametuma salaam za rambirambi kwa wananchi wa Hanangi Pamoja na kutoa maelekezo kwa wizara zote za kisekta kushughulikia changamoto hiyo.

 

Tayari Mawaziri kadhaa wamewasili Hanang kuongoza wananchi kuwasaka wahanga wa mafuriko hayo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa, pamoja na Wakuu wa Vyombo vya ulinzi na Usalama wamefika katika kijiji cha Gendabi kata ya Gendambi Wilaya ya Hanang mkoani Manyara eneo yalipotokea mafuriko ambayo yamesababisha vifo vya watu, majeruhi na uharibifu mkubwa wa Miundombinu mbalimbali, yakiwamo mashamba na makazi ya wananchi.

Mapema leo Viongozi hao wameongozwa na Mkuu wa Mkoa Manyara, Queen Sendiga kufika katika Kijiji cha Gendabi ambalo ni eneo lililoathirika sana na Maporomoko ya Matope kutoka Mlima wa Hanang yaliyotokea usiku wa kuamkia tarehe 03 Disemba 2023.

 

Waziri Mkuu kassim majaliwa akizungumza na iongozi wa mkoa wa manyara pamoja na kamati ya maafa baada ya kuwasiri mkoani humu kuratibu shughuli za uokoaji.

Waziri MKUU Kassim majaliwa muda mfupi uliopita naye amewasili mkoani manyara ambapo amekagua shughuli za uokoaji na urejeshaji wa hali katika maeneo yaliyoathirika na kuwahimiza viongozi wa mkoa na wizara kushughulikia kila changamoto itakayoibuka kutokana na janga hilo

Aidha ametangaza kuwa serikali itagharimia mazishi kwa marehemu wote sambamba na kutoa huduma zote kwa wahanga ambao wamelazimika kuwa wakimbizi katika meneo yao kufuatia kubomoka kwa nyumba zao.

Wakati huo huo Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana, amewahakikishia wananchi wilayani Hanang Mkoa wa Manyara hususan waliokumbwa na janga la mafuriko, kwamba maelekezo ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, yatatekelezwa kikamilifu na idara na taasisi zote kama walivyoagizwa chini ya usimamizi wa Waziri Mkuu

 

Kinana ameyasema hayo leo Desemba 4, 2023 alipowatembelea waathirika wa mafuriko hayo katika baadhi ya vijiji vya Wilaya ya Hanang.

 

Kinana amewatembelea na kuwafariji wananchi waliopoteza ndugu zao na waliojeruhiwa na kulazwa hopitalini kutokana na janga hilo ambapo amewapa pole na kuwaomba wawe na subira katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana,Akiwapa pole Wakazi wa Kata ya Gendambi alipowatembelea waathirika wa mafuriko hayo katika baadhi ya vijiji vya Wilaya ya Hanang.

 


Post a Comment

0 Comments