Waziri Makamba ateta na Katibu mkuu AfCFTA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) amekutana na kuzungumza na Katibu Mkuu wa Secretarieti ya Soko Huru la Pamoja Barani Afrika (AfCFTA), Bw. Wamkele Mene katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

Bw.Wakele Mene yupo nchini kuhudhuria Kongamano la Pili la AfCFTA la Wanawake katika Biashara lililofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 6-8 Disemba, 2023 na kukutanisha wanawake walioko katika biashara kutoka nchi mbalimbali barani Afrika .


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb.) akizungumza na Katibu Mkuu wa Secretarieti ya Soko Huru la Pamoja Barani Afrika (AfCFTA) Bw. Wamkele Mene walipokutana katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamejadili juu ya namna bora ya kuendesha biashara katika bara la Afrika kupitia soko hilo la AfCFTA.

Mhe. Waziri Makamba amemuhakikishia Bw. Wamkele Mene kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kushirikiana na AfCFTA katika kuhakikisha soko hilo linaleta manufaa yaliyokusudiwa.

Mwandishi: Foreign Tanzania

Mhariri: Adela Madyane


Post a Comment

0 Comments