Dr. Mpango awafunda vijana wa UVCCM dhidi ya mitandao


Wakati Vijana wa CCM wakikutana mkoani Kigoma kujadili mstakabali wa taifa, Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango amewaasa vijana kutumia vizuri mitandao ya kijamii huku akiwaonya kutokukubali kutumiwa kisiasa katika kuchochea vurugu kwa  kushirkii kwenye maandamano na vurugu sisizo na tija


Aliyasema hayo katika kongamano la kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan na maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) yalifanyika kitaifa hapo jana katika viwanja vya Kawawa vilivyopo manispaa ya Kigoma Ujiji 


"Vijana mnapaswa kuwa kielelezo cha uadilifu, mlinde mila na desturi, mtumie mitandao ya kijamii kuongeza maarifa ili kuleta tija na utatuzi juu ya masuala mbalimbali katika jamii na si kutumia mitandao kuchafuana,kupotosha, na kuleta taharuki katika jamii" Amesema Mpango.

Dkt Mpango makamu wa Rais akisalimia wananchi katika uwanja wa kawawa ujiji mkoani Kigoma alipowasili kushiriki kongamano la vijana la kumpongeza rais Samia

Dkt Mpango aliwasisitiza vijana kutumia majukwaa rasmi ya kufikisha maoni yao kwaajili ya kupata suluhu na si kuandamana kwani maandamano sio suluhu kwa kila kitu.


"Uchumi wa dunia umeathirika na ugonjwa wa Covid 19, Vita vya pamoja na vita vinavyoendelea ukanda wa Mashariki ya kati,  athari hizi haziwezi kutatuliwa kwa mara moja tena kwa maandamano , vijana msikubali kutumika' Alisisitiza Mpango 


Alisema Rais Samia anataka usawa na watu wote waheshimiane, wawe wastahimilivu na kuepuka migogogro na pale inapobidi suluhu itafutwe mara moja ili kuleta mageuzi ya kukuza nchi na kwamba nchi inaendelea kupambana kwaajili ya kutatua changamoto zilizopo

Baadhi ya wajumbe wa Barala la vijana Taifa wakisikiliza hotuba ya makamu wa Rais katika uwanja wa Kawawa Ujiji mkoani Kigoma

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa kamishna generali wa zimamoto mstaafu Thobias Andengenye amemshukuru Rais Samia kwa kutimiza ahadi yake ya kufungua mkoa wa Kigoma katika ziara aliyoifabya Oktoba 2022kwa kufanya kuwa kitovu cha biashara ambapo kwa kipindi cha miaka mitatu mkoa umepokea trilioni 11.450 zilizoelejezwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo


"Kwanza Kuna mradi wa umeme katika mto Malagrasi eneo la Igamba lenye kw 45.6, kuunganisha umeme mkubwa kutoka Rusumo, kuanzia Nyakanazi mpaka Kidahwe takribani kilomita 280, umeme wa msongo KV 400 utatoka huko mpaka Kigoma, na unatarajiwa kukamilika mwezi wa nne mwaka huu, mradi wa SGR kutoka Tabora wenye urefu wa kilomita 506, kujenga reli ya Uvinza -Msongati wenye gharama ya tririoni 1.74, kukarabati meli ya mafuta ya Mv Sangara,  na ujenzi wa meli za mizigo, ujenzi wa kiwanda cha kutengenezea meli pamoja na kudumisha huduma za afya" Alisema Andengenye.

Comrade Rehema akiteta jambo na Katibu mkuu wa UVCCM Taifa katika ofisi za Wakala wa Meli Tanzania walipotembelea bandari ya Kigoma kushuhudia maboresho na matengenezo ya Meli ya MT Sangara na MV Liemba

Naye Rehemu Sombi makamu mwenyekiti wa UVCCM alisema serikali ya awamu ya sita imekuwa kinara cha demokrasia kwa kuimarisha na misingi ya utu, kuhimiza haki, usawa na uongozi bora jambo ambalo linadumisha amani na mshikamo wa taifa letu.


"Juzi chama ndugu kimojawapo kuliweza kufanya maandamano ambayo kipindi cha nyuma hayakuweza kuruhusiwa lakini wamepewa ulinzi wa kutosha, na hii inaonesha kuwepo kwa  ukomavu ya kidemokraisa, iliyohuishwa katika awamu hii ya uongozi" alisema Sombi.

Awali viongozi wa jumuia ya vijana ya CCM taifa walifanya ziara katika miradi mbalimbali ya maendeleo na kufanya mikutano katika wilaya zote za mkoa wa Kigoma.


Mwenyekiti wa UVCCM taifa Comrade Mohamed Kawaida akisalimiana na Mbunge wa Vijana kutoka mkoa wa Kigoma Mhe. Sylvia walipokutana mjini Kigoma kwa ajili ya Kongamano la kupongeza Rais Samia Suluhu hassan kwa uongozi wake wa miaka mitatu (3) 



 

Post a Comment

0 Comments