Breaking News; UTEUZI NA UTENGUZI, Makonda RC Arusha



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuziutenguzi na uhamisho waviongozi kama ifuatavyo:

 

i) Amemteua Mhe. Deogratius John Ndejembi (Mb.) kuwaWaziri wa NchiOfisi ya Waziri Mkuu (KaziVijanaAjira na Wenye Ulemavu).

Kabla ya uteuzi huu Mhe. Ndejembi alikuwa NaibuWaziri wa NchiOfisi ya Rais – Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa (TAMISEMI). Mhe. Ndejembianachukua nafasi ya Mhe. Prof. Joyce Lazaro Ndalichako ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

 

ii) Amemteua Bw. Paul Christian Makonda kuwa Mkuu waMkoa wa Arusha. Kabla ya uteuzi huu BwMakondaalikuwa Katibu wa ItikadiUenezi na Mafunzo waChama cha Mapinduzi (CCM). Anachukua nafasi yaMhe. John  Vianney Mongella ambaye atapangiwakazi nyingine.

 

iii) Amemteua Kanali Evans Alfred Mtambi kuwa Mkuuwa Mkoa wa Mara. Kabla ya uteuzi huu KanaliMtambi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga.

 

iv) Amemhamisha Mhe. Said Mohamed Mtanda kutokaMkoa wa Mara kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa waMwanza. Mhe. Mtanda anachukua nafasi ya Mhe. Amos Gabriel Makalla ambaye atapangiwa kazinyingine.

 

v) Amemteua Mhe. Zainab Athuman Katimba (Mb.) kuwaNaibu Waziri wa NchiOfisi ya Rais – Tawala za Mikoa ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Mhe. Zainab anachukua nafasi ya Mhe. DeogratiusJohn Ndejembi (Mb.) ambaye ameteuliwa kuwaWaziri.

 

vi) Amemteua Mhe. Daniel Baran Sillo (Mb.) kuwa NaibuWaziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Mhe. Silloanachukua nafasi ya Mhe. Jumanne Abdallah Sagini(Mb.) ambaye amehamishwa kwenda kuwa NaibuWaziri wa Wizara ya Katiba na Sheria. 

 

vii) Amemhamisha Mhe. Mhandisi Maryprisca Winfred Mahundi (Mb.) kutoka Wizara ya Maji kwenda kuwaNaibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano naTeknolojia ya Habari.

 

viii) Amemhamisha Mhe. Kundo Andrea Mathew (Mb.) kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojiaya Habari kwenda kuwa Naibu Waziri wa Wizara yaMaji.

 

ix) Amemteua BwFakii Raphael Lulandala kuwa Mkuuwa Wilaya ya SimanjiroKabla ya uteuzi huu BwLulandala alikuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijanawa Chama cha Mapinduzi (UVCCM).

 

x) Amemteua Bw. Gilbert Kalima kuwa Mkuu wa Wilaya ya MkingaKabla ya uteuzi huu BwKalima alikuwaKatibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi.

 

xi) Amemhamisha Mhandisi Cyprian John Luhemejakutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (KaziVijana na WenyeUlemavukwenda kuwa Katibu MkuuOfisi yaMakamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

 

xii) Amemhamisha Bi. Mary Ngelela Maganga kutokaOfisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingirakwenda kuwa Katibu MkuuOfisi ya Waziri Mkuu(KaziVijanaAjira na Wenye Ulemavu).

 

xiii) Amemteua Dkt. Edwin Paul Mhede kuwa NaibuKatibu MkuuWizara ya Mifugo na UvuviDktMhede aliwahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala waMabasi Yaendayo Haraka (DART). 

DktMhede anachukua nafasi ya Bi. Agnes KisakaMeena ambaye amehamishwa kuwa Naibu KatibuMkuuWizara ya Maji.

 

xiv) Amemteua Dkt. Suleiman Hassan Serera kuwa NaibuKatibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa naMichezoKabla ya uteuzi huu DktSerera alikuwaMkuu wa Wilaya ya Simanjiro

DktSerera anachukua nafasi ya BwNicholausMkapa ambaye amehamishwa kwenda kuwa NaibuKatibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano naTeknolojia wa Habari.

 

xv) Amemteua BwSelestine Gervas Kakele kuwa BaloziKabla ya uteuzi huu BwKakele alikuwa NaibuKatibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano naTeknolojia ya Habari.

   

xvi) Amemteua Balozi Dkt. Asha Rose Migiro kuwaMjumbe wa Tume ya Mipango

 

Uapisho wa Waziri, Wakuu wa MikoaNaibu Mawaziri naNaibu Makatibu Wakuu utafanyika tarehe 04 Aprili, 2024 saa05:00 asubuhi Ikulu, Dar es Salaam.

 

Post a Comment

0 Comments