Dr. Samia Ahimiza Wanawake wapewe nafasi za Uongozi

Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa taasisi za kiserikali na sekta binafsi kufanya jitihada za kuhakikisha wanawake wanapata nafasi na kusikika kwenye maamuzi mbalimbali nchini.

Rais Samia amesema hayo leo kwenye mkutano wa wanawake walio katika sekta ya fedha uliofanyika  ukumbi wa hoteli ya Kwanza iliyopo Kizimkazi. 

Aidha, Rais Samia amesema ushiriki wa wanawake kwenye ngazi za maamuzi ni suala jumuishi na endelevu hivyo halipaswi kuchukuliwa kama la kimapinduzi au la serikali pekee. 

Rais Samia amebainisha kuwa lengo ni kuhakikisha masuala yanayowahusu wanawake ambayo wafanya maamuzi wengine wanaweza wasiwe na uelewa nayo yanapata nafasi kwenye meza ya maamuzi. 

Hali kadhalika, Rais Samia amesema pamoja na kuongeza ushiriki wa wanawake kwenye ngazi za maamuzi lazima pia kuweka nguvu kubwa katika kuwainua wanawake kiuchumi.

Kwa upande mwingine, Rais Samia amewataka wanawake kujipanga na kufikia malengo yao kwa vitendo. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA), Kizimkazi, Zanzibar, tarehe 14 Machi, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na viongozi wengine wakati wa Tamasha la Wanawake Sekta ya Fedha Kizimkazi, Zanzibar tarehe 14 Machi, 2024
 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mama Fatma Karume Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume mara baada ya kuhutubia na kuzindua Chama cha Wanawake Sekta ya Fedha Tanzania (TAWiFA) Kizimkazi, Zanzibar tarehe 14 Machi, 2024. 

Post a Comment

0 Comments