Mabadiliko ya tabianchi yawaliza wanawake Kigoma


Wanawake wilayani Kasulu mkoani Kigoma wameiomba selikali kupunguza bei ya gesi ili  kuondoa  madhila yanayowakabilii wanawake mkoani Kigoma wakati wa utafutaji wa kuni na mkaa.  

Rai hiyo imetolewa na  baadhi ya wananchi wa mjini Kasulu wakati  wakizungumza na Buha News leo hii wakati wa kipindi cha wanawake na tabianchi.

Akizungumza katika majadiliano   Bi. Leonia Kimena ambaye ni mfanyabiashara za chakula maarufu “mama lishe”, amesema wanawake wamekuwa wakikumbwa na changamoto nyingi wakati wakutafuta kuni na mkaa ikiwemo kutishiwa kubakwa na kuporwa. 

Amesema kuwa wanawake wengi hasa wa kipato cha chini hutumia mda mrefu kutafuta nishati ya kupikia na kupelekea kuleta migogoro katika ndoa zao pamoja na magonjwa yatokanayo na moshi au vumbi la mkaa. 

Bi. Leonia Kimena (kushoto) mama lishe Kasulu, Sara Mataro (katikati) mwanndishi wa habari na Bw. Alex Kayanda (kulia) katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mahojiano. 

Bi. Kimena amesema baadhi familia wanaume hawaamini  kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaweza kusababisha matumizi makubwa ya mda kutokana na misitu kuharibiwa na shughuli za binadamu na kupungua kwa miti inayotumiwa na jamii kwa ajili ya nishati ya kupikia. 

Akijibu hoja hizo Alex Kayanda mkazi wa wilaya ya kasulu ambaye pia ni baba lishe, amethibitisha kuwepo kwa hali hiyo ya migogoro katika baadhi ya familia inayotokana na uhaba wa nishati safi ya kupikia hususani gesi. 

Bw. Kayanda ambaye pia ni Baba lishe ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa wanaume kujenga tabia ya kuwaamini na kuwasaidia wake zaoo katika shughuli za nyumbani ikiwemo kununua gesi ili kuwaepusha na hatari zinazoweza kuwakuta wawapo katika harakati za kutafuta kuni porini

Kayanda amesisitiza kuwa, uharibifu wa mazingira unaodhihirishwa na mabadiliko ya tabianchi unasababisha Maisha kuwa magumu kwa jamii na kutoa wito kwa serikali kutoa elimu itakayosaidia wananchi kupunguza uharibifu wa mazingira sambamba na kurahisisha upatikanaji wa nishati mbadala 

Utegemezi wa Matumizi ya kuni na mkaa imetajwa kua miongoni mwa vyanzo vya uharibifu wa mazingira vinavyo pelekea mabadiliko ya tabia nchi .ambayo huwa na athari nyingi zikiwemo na ukame au mafuliko Pamoja na joto kali. 

Kigoma ni miongoni mwa mikoa ambayo bado ina ardhii oevu na misitu asilia inayochangia upatikanaji wa hewa safi na kupunguza hewa ukaa,, hata hivyo hivi karibuni kueripotiwa kuwepo kwa uvamizi mkubwa wakulima na wafugani katika misitu iliyohifadhiwa.


https://on.soundcloud.com/1AvYD

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments