Rudisheni mikopo ya asilimia 10 tujikomboe - wanawake Kigoma

Wanawake mkoani Kigoma wameiomba selikali kurudishwa mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya halimashauri kwa ajili ya wanawake ,vijana na walemavu kujengewa uwezo wa kiuchumi. 

Ombi hilo limetolewa na  wa umoja ummoja wa akina mama  wakati wa maadhimisho ya siku ya wananwake duniani ambayo kimkoa yalifanyika kata ya Makere wilayani Kasulu march 8 ambapo wadau mbalimbali walihudhuria.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa mkoa wa kigoma mh Thobias Andengenye, mwakilishi wa wanawake hao Bi. Zuena Hassani ambaye ni mwanachama wa kikundi cha Malezi Chanya alisema  kuwa, kusitishwa kwa mikopo hiyo imekua pigo kubwa kwa wanawake wa mkoa wa Kigoma katika kutatua changamoto za maisha zinazowakabiri. 

Alisisitiza kuwa wanawake wengi wameshindwa kufanya shughuli za kijamii kutokana na kukosa mitaji hali inayo pelekea kuwa na maisha duni na kuporomoka kwa maendeleo ya kijamii. 

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh. Thobias Andengenye akihutubia wanawake katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake kimkoa yaliyofanyika katika kijiji cha Makere wilayani Kasulu March 8, 2024. Picha na Sara Mataro

Akijibu risala hiyo mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Kigoma Mh. Thobias Andengenye    amesema changamoto hiyo ya kurejeshewa kwa mikopo  inayotokana na ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri ameichukua  na ameahidi kuitatua 

Mh. Andengenye ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa wanawake kuchangamkia fursa za kazi na kujiajili katika sekta isiyo  rasmi kwa kutekeleza sshughuli mbalimbali kama vile kilimo na ufugaji. 

Amesisitiza kuwa  nje ya mikopo  ya asilimia nne kwa kina mama, ipo mikopo itolewayo na taasisi zisizokua za kiserikali ambapo wanawake wanawezeshwa na kufundishwa  namba ya kubuni na kusimamia miradi yao 

Katika kusherehekea siku ya wanawake duniani, Mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye alitoa vyeti kwa baadhi ya vikundi vya akina mama wa mkoa wa kigoma vilivyofanya vema ili kuvipa motisha ya kufanya kazi kwa juhudi na kuepuka kuwa tegemezi katika familia. 

Mbunge Viti Maalumu mkoa wa Kigoma Mh. Josephine Genzabuke (kushoto) ni miongoni mwa walioshiriki maadhimisho ya siku ya wanawake duniani mkoani Kigoma. Picha na Sara Mataro.

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani huazimishwa kila mwaka march 8 ambapo katika mkoa wa Kigoma yameazimishwa katika kata ya Makere wilayani kasulu chini ya  kauli mbiu “Wekeza kwa mwanamke ili kuharakisha maendeleo kwa taifa na jamii.

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments