Toeni mafunzo stahiki kwa vijana kujiajiri na si kuomba ajira- RC Kigoma

 


Mkuu wa mkoa wa Kigoma Mh. Thobias Andengenye avitaka Vyuo vya ufundi kutoa mafunzo na ujuzi utakaowasaidia wahitimu kujiajiri badala kutegemea kuomba ajira

Amesema hayo wakati akizindua Makala maalumu iliyotengenezwa na Chuo cha maendeleo ya wananchi (FDC) Kasulu ikionesha namna wasichana wanavyoweza kujiajiri baada ya kupata mafunzo katika chuo hicho.

Mh. Andengenye amesema vyuo vinavyotoa mafunzo ya ufundi havina budi kutaathimini ufundishaji wao na kuhakikisha wanazalisha wataalumu watakaobuni na kutekeleza miradi na kuwaajiri wenzao badala ya waomba ajira

Rai yangu kwenu mimi nimekuwa nikipokea simu nyingi sana kutoka kwa vijana ambao wamesoma VETA na wengine vyuo vya maendeleo ya wananchi kama hicho cha kwenu wakitaka niwasaidie kutafuta kazi, hivi vitu viwili vinachanganya, mimi ninaomba watu wanaotoka FDC na VETA wasiwe wanatafuta ajira badala yake watafute kazi” anahimiza mkuu wa Mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye

Amesisitiza kuwa ajira ziko chache ukilinganisha na kazi na kwamba Tanzania haijawahi kuwa na changamoto ya kazi bali ajira ukilinganisha nan chi za Jirani ambako hata kupata kazi ni vigumu

Sisi tunajua Ninyi mnazalisha wakurugenzi wanaokuja kuongeza ajira siyo kuomba ajira, kuanzia mwanzo wakifika watambue kuwa wao ni wataalamu waajiri wataarajiwa wanaokuja kuongeza ajira, wakimaliza vyuo wakawaajiri wengine ambao hawana ujuzi kama wao” amesisitiza.

Amebainisha kuwa serikali inatoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu kutoka katika asilimia kumi za mapato ya Halmashauri ambao hukopeshwa ili kuwajengea uwezo katika miradi yao ili wawaajiri wengine

Sehemu ya Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Kasulu, kinapokea wasichana waliokatishiwa masomo pamoja na makundi mengine ya vijana 

Mkuu wa chuo cha maendeleo Kasulu Mwl. Fridegarda Mukyanuzi akitoa taarifa kwa mkuu wa mkoa aliyetembelea bada la chuo hicho alibainisha kuwa FDC inatoa mafunzi mbalimbali kwa vijana hususani wasichana na wanawake waliokatisha masomo ya sekondari kwa sababu mbalimbali

Mwl. Mukyanuzi alibainisha kuwa kupitia katika kozi zitolwazo katika chuo hicho wasichana wameonesha mwamko wa kujifunza fani za Umeme, Uashi, uselemara, mapambo na urembo na kwamba Makala ya video iliyoandaliwa inaonesha shuhuda mbalimbali.

Chuo cha maendeleo ya wananchi (FDC) Kasulu kinatoa mafunzo ya ufundi stadi na teknolojia ya Habari na mawasiliano (TEHAMA) kupitia kozi fupi na ndefu kwa kushirikiana na taasisi ya Karibu Tanzania Association (KTO) ambao ni asasi ya Pamoja kati ya Tanzania na Sweeden wanao saidia mabinti waliokatishwa masomo kwa sababu mbali mbali kurejea shuleni kwa kupewa elimu maalumu.

Sehemu ya Chuo cha VETA Kasulu kilichoko eneo la Nyumbigwa

Aidha huo cha mafunzo ya Ufundi VETA Kasulu nacho hupokea vijana na kutoa mafunzo mbalimbali ya ufundi, sayansi na teknolojia ili kuwajengea uwezo vijana kupata ujuzi mbalimbali utakaowawezesha kukuza uchumi binafsi na taifa.

Imeandikwa na: Sara Mataro

Imehaririwa na. Prosper Kwigize

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments