Rai hiyo imetolewa
na Mhasham Askofu Josephu Romani Mlola
wa jimbo la Kigoma April 21 wakati wa
misa takatifu ya dominika ya 4 iliyo azimishwa katika parokia ya teule ya Mwilamvya Kasulu Jimbo la Kigoma ikiwa
ni wiki ya kuombea miito mitakatifu
Amefafanua kuwa kuna umuhimu mkubwa pia wa kuombea miito
ya ndoa takatifu kwani ndio muito pekee
unao leta matokeo ya miito mikubwa ya
upadre na utawa hivyo ili kupata Baraka katika maisha ya kiroho na kimwili.
Amesema wazazi wanayo nafasi kubwa ya kuilea miito
hiyo katika malezi ya Watoto kwa maadili ili kutengeneza miito miingine ya
kiroho hususani wito au sakrament ya upadre na utawa
Askofu Mlola
amehimiza wazazi na jamii kutoacha jukumu la mazlezi ya Watoto kwa wasichana wa
kazi (watumishi wa nyumbani) fuatilia nyendo za watoto wao na sio kuwaachia na
kuwaamini wadada wa kazi bali kulinda familia na kuwa mchungaji bora katika
familia.
Wakati huo huo
Askofu Mlola ametumia Misa hiyo kutoa wito kwa watanzania wote kuzingatia amani
wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu Pamoja na uchaguzi mkuu wa
mwaka 2025 kwa kuchagua viongozi wenye maadili na kuonya wanaoanza kuleta chokochoko
kwa kutoa kauli zinazochochea uvunjifu wa amani
Mwandishi: Sara Mataro
0 Comments