Mbunge wa Jimbo la
Bukoba Vijijini mkoani Kagera Dkt
Jasson Samson Rweikiza amesema kwa
kipindi cha miaka 3 (2021_2023) miradi mingi ya Maendeleo imetekelezwa hasa kwenye sekta za Miundombinu ikiwemo Barabara,
Elimu
na Afya kwa kata zote za Jimbo hilo.
Dkt Rweikiza amesema
hayo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi cha miaka 3
wakati wa kikao cha kawaida cha Halmashauri kuu ya Chama hicho wilaya ya Bukoba
Vijijini ambacho kimefanyika April 20 katika Jimbo hilo.
Ametaja baadhi ya
miradi iliyotekelezwa katika jimbo hilo kwa kipindi hicho
kuwa ni pamoja na miradi ya Barabara ambapo kwa mwaka wa Fedha 2020/2021
miradi 52 ya Barabara katika kata 29 zilifanyiwa
matengenezo ya mara kwa mara , utengenezaji maeneo korofi pamoja na matengenezo ya madaraja madogo ikiwa na thamani ya
zaidi ya shilingi bilioni 1, na
kwamba Mwaka
2021/2022 Miradi 50 ya Barabara yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 2
ilitekelezwa katika kata 29.
Ameongeza kuwa kwa
mwaka wa Fedha 2022/2023 miradi ya
Barabara 48 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1 katika kata 29
imetekeleza na kwa mwaka wa fedha 2023/2024 mpaka taarifa hiyo inaandaliwa
miradi 4 kati ya 52 ya barabara ambayo inatekelezwa ilikuwa imekamilika ambapo
miradi 48 inaendelea na ukarabati na mingine iko katika hatua za manunuzi na fedha zote zinatoka katika mfuko
wa barabara , Fedha za Jimbo na tozo za mafuta ili kukamilisha kazi.
Dkt. Rweikiza amebainisha kuwa miradi
mingine iliyotekelezwa katika Jimbo hilo ni miradi ya afya na Elimu ambapo
zimejengwa Zahanati na kuboresha huduma za afya na wanaendelea na ujenzi wa
kituo cha afya katika kata ya Rukoma sambamba na ujenzi wa shule mpya za
msingi na sekondari
Amesema kuwa katika kipindi hicho
pia miradi ya maji imetekelezwa katika kata ya Kagya, Katoma, Karabagaine , Kemondo, Katerero na
Bujugo akieleza kuwa
mafanikio hayo
ni kutokana na ushirikiano mkubwa kutoka kwa wananchi, Serikali pamoja na Mbunge huku akimshukuru Mh Rais Dkt Samia Suluhu
Hassan kwa kuleta fedha nyingi ya utekelezaji wa miradi mikubwa katika Jimbo
hilo.
Kwa upande wake Mwenyekiti
wa chama cha Mapinduzi mkoa wa Kagera Nazir Karamagi aliyekuwa mgeni Rasmi katika kikao hicho amewataka
wanachama wa chama hicho kuwapa ushirikiano viongozi walioko madarakani na
kutowasumbua kwani kipindi cha uchaguzi bado isipokuwa wawape ushirikiano ili
waweze kutekeleza ilani ya chama hicho kama walivyowaaidi wananchi .
Naye mjumbe wa
halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi
Taifa (MNEC) Bwana Kharim Hamri amewataka wanachama wa
chama hicho kuwapuuza watu wanaotafuta madaraka kwa mafarakano au misingi ya
udini na ukabila kwani hatowafaa kuwa kiongozi wao na kuongeza kuwa chama hicho
kiko imara na viongozi wake wanaendelea kufanya kazi kwa weledi mkubwa ili
kuwaletea wananchi maendeleo.
Mwandishi: Mariam Kagenda
Mhariri: Prosper Kwigize
0 Comments