Kilimo katika vyanzo vya maji kuhatarisha uhai wa mito Kasulu


Wakulima wadogo wadogo wa kilimo cha umwagiliaji katika bonde la mto Bogwe mjini Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kufata kanuni za kilimo bora ili kuzuia uchafuzi na uhalibifdu wa vyanzo vya maji unaoweza kusababisha ukame.

Hayo yamesemwa na Afisa wa mamlaka ya maji mjini Kasulu Bw. John Mikidadi wakati wa mahojiano na Buha News ofisini kwake kuhusu uchafuzi wa mito unao jitokeza katika nyanzo vya maji.

Amesema baadhi ya wakulima wanafanya shughuli za kilimo kando kando ya vyanzo vya maji hali inayo pelekea uhalibifu wa mazingira na kusababisha maji kutoka katika mabomba yakiwa machafu.

Ameeleza kuwa kilimo kando kando ya mto athari yake ni kupungua kwa chanzo cha maji na kusababisha madawa ya kilimo kuingia mitoni na kuhatarisha usalama wa watumiaji wengine wa maji

Bw. John Mikidadi afisa maji katika mamlaka ya maji mjini Kasulu

Dawa zitumikazo shambani hasa za kisasa kwenye kilimo cha umwagiliaji zina madhara mengi kwa viumbe na pia kuchangia kuwepo kwa mabadiliko ya tabia nchi” amesisitiza Bw. Mikidadi

Bw. Mikidadi ametumia fursa hiyo kutoa rai kwa wakulima katika maeneo ya mito na vyanzo vya maji kufuata kanuni na ushauri unao tolewa na maafisa wa kilimo na kuacha umbali wa mita 60 kutoka katika mto na kutumia vifaa vya kisasa ili kuepusha uchafuzi unajiotokeza  

Kwa upande wake mmoja wa wakulima wa maeneo ya hayo Bw. Amos Ndikulije amekiri kuwepo na uharibifu sambamba na ukiukwaji wa sheria za mazingira na ameiomba serikali kuongeza maafisa kilimo ili kutoa elimu ya kutosha juu ya kilimo bora.

Amesema wakulima wengi wamekuwa wakichafua vyanzo vya maji na hata kusogeza mashamba yao karibu na mto pasipo kujua madhara yanayo weza kujitokeza

Bw. Yese Ndiliwe ambaye ni mkulima mkongwe katika bonge la mto Bogwe amesema wakulima hufata vyanzo vya maji ili kurahisisha shughuli za umwagiliaji

Ameongeza kuwa wakulima wengi wanashindwa kununua pambu za kisasa kwa ajili ya umwagiliaji kutokana na kipato duni

Mmoja wa wakulima katika bonde la mto Bongwe uliopo mjini Kasulu mkoani Kigoma

Akijibu malalamiko hayo afisa kilimo wa kata ya Mwilavya Bi. Evita Rupeche amekiri kuwepo kwa changamoto ya uharibifu wa vyanzo vya maji vitokanavyo na wakulima kunakotokana na wakulima kukaidi maelekezo ya serikali

Amebainisha kuwa ofisi yake imekuwa ikitoa elimu kwa njia mbalimbali ikiwemo kusambaza machapisho yanayoelekeza kuhusu kilimo bora na endelevu

Uchafuzi na uharibifu wa vyanzo vya maji ni moja ya sababu za mabadiliko ya tabia nchi

Mji wa Kasulu jina lake hupambwa na mto Kasulu ambao umebaki historia kufuatia kukauka kwa chanzo chake huku Mto Bogwe uliokuwa mkubwa na watu wakivuka kwa mitumbwi miaka ya 1980 uko katika hatari ya kutoweka.

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

 

Post a Comment

0 Comments