Mabalozi wa CCM waguswa na utendaji wa Profesa Ndalichako

 

Wenyeviti wa mashina wa Chama Chama Mapinduzi wilayani Kasulu mkoani Kigoma wamemshukuru Mbunge wa jimbo la Kasulu Mjini Profesa Joyce Ndalichako kwa kutambua umhimu na mchango wa viongozi wa mashina kwa kuwakutanisha pamoja katika mafunzo ya kuwawezesha kujua wajibu na nafasi zao katika chama.

Shukurani hizo zimetolewa na mabalozi zaidi ya 400 mwishoni mwa juma lililopita baada ya kupata mafunzo ya kuwajengea uwezo kuelekea uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu

Mwamini Shem Kazara ni mwenyekiti wa shina namba 5 kata ya Murubona ni mmoja wa amesema mbali na kuwa na changamoto nyingi katika mashina wamefuraishwa na kitendo cha mbunge kugharimia mafunzo hayo

Aidha Mwamini amekipongeza Chama Cha mapinduzi kwa kuahidi kuanza kuwalipa posho viongozi wa mashina maarufu kama Mabalozi kutokana na fedha zalipo ya ada ya mwanachama.

Amefafanua kuwa fedha hizo zitsaidia kufanya mabadiliko makubwa katika uongozi wa mashina kama vile kununua mahitaji mbalimbali.

Baadhi ya Mabalozi kutoka kata ya Murusi mjini Kasulu wakipiga makofi kumpongeza mbunge wao kwa kitendo cha kuwaleta pamoja na kushiriki mafunzo ya uongozi na uchaguzi

Kwa upande wake Katibu Itikadi siasa na Uenezi wa CCM kata ya Murusi ndg. Adriani Ndorere amesema mkutano huu umewapa chachu na motisha wenyekiti wa shina ambao wamekuwa wakifanya kazi kwa kujitolea na kukisaidia chama kupata ushindi

“Mabalozi walikuwa hawalipwi chochote walifanya kazi kama wakereketwa wa chama na sasa Raisi Samia Suruhu Hassani ametambua mchango wao” aliongeza Ndg Ndorere

Awali, Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma ndugu Mobutu Malima alitangaza kuwa Chama makao makuu kimenunua pikipiki kwa ajili ya watendaji wake ngazi ya kata na kwamba hivi karibuni zitagawiwa ili kuwawezesha viongozi hao kufanya kazi kwa weledi.

Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma ndg Mobutu Malima (kushoto) akifuatilia kwa makini utambulisho wa mafunzo kwa kwa ajili ya viongozi wa Chama hicho ngazi ya Shina

Bw. Malima alibainisha kuwa viongozi watakaonufaika na mpango huo ni makatibu wa jumuiya zote Pamoja na makatibu kata wa Chama.

“Mjiandae kupokea pikipiki na mkazitumie kwa shughuli za chama na siyo kufanya biashara ya bodaboda, na pia nawahimiza mkapate mafunzo ya udreva katika taasisi za mafunzo ili kupata ujuzi na mhakikisha mnapata leseni za kuendesha vyombo vya moto” Alisisitiza Malima.

Hii ni mara ya kwanza kwa mabalozi wa nyumba kumi ngazi ya jimbo kukutanishwa na kupewa mafunzo ya wajibu wao kwa mujibu wa katiba ya CCM katika wilaya ya Kasulu na mkoa wa Kigoma.

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments