Mama Lishe Kasulu waonywa kuzingatia usafi wa mazingira

 

Wafanyabiashara wa chakula mjini Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kusafisha mazingira yanayo wazunguka kwa kuweka maji tililika kwa ajili ya usafi wa mikono ili kuzuia magonjwa ya mlipuko.

Agizo hilo limetolewa na afisa afya na mazingira wa halmashauri ya Mji wa Kasulu Bw Msafiri Charles wakati wa mahojiano na Buha News ofisini kwake kuhusu kampeni ya usafi wa mazingira iliyoanzishwa April mosi mjini Kasulu.

Amesema ni wajibu wa kila mjasiliamali wa chakula kufanya biashara kwa kuzingatia ubora wa afya kwa mteja wake.

Ameeleza kuwa baadhi ya wajasiriamali wanafanya biashara bila kuweka vifaa sahihi vya kusafishia mikono na wengine kusogeza biashara za chakula karibu na dampo la uchafu bila kujali madhara yatakayo jitokeza.

Mmoja wa mama lishe katika eneo la Mnadani mjini Kasulu mkoani Kigoma

Amebainisha kuwa athari za uchafu ni pamoja na magonjwa ya mlipuko ikiwemo na kipindu pindu na homa za mtumbo yanayo pelekea upotevu wa maji mwilini

Sambamba na hilo Bw. Msafiri ameelekeza uongozi wa kila kata kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara wasio kuwa na vifaa vya kutunzia uchafu na  wanao fanya biashara sehemu hatarishi.

Kwa upande wake Happiness Nkone ambaye ni mjasiliamali mkongwe wa chakula eneo la Mnadani amekiri kuwepo kwa mulipuko wa magonjwa yanayotokana na kula chakula kichafu

“Tunashindwa kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya usafi sio kwamba atujui apana lakini ni mtaji mdogo hivyo kulazimika wateja wetu kunawa kwenye chombo kimoja” amesema Happiness

 

Post a Comment

0 Comments