Marais wa Afrika waipongeza Tanzania- miaka 60 ya Muungano

 

Marais kutoka nchi za jumuiya ya maendeleo kusini mwa Afrika na jumuiya ya Afrika mashariki wameipongeza Tanzania kwa kuwa na muungano wa kipekee duniani ulioziunganisha Tanganyika na Zanzibar.

Pongezi hizo zimetolewa na Rais wa Jamhuri ya Burundi Sylvestre Ndayishimiye Pamoja na Rais wa Comoro Azali Assoumane wakati wa sherehe za kilele cha maadhimisho ya siku ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam

Marais hao kwa Pamoja wakiwawakilisha wengine wameishukuru Tanzania kwa mchango mkubwa iliyoutoa wakati wa harakati za kupigania uhuru wa mataifa yao Pamoja na ushirikiano wa kiuchumi unaoendelea baina ya nchi za SADC na Afrika kwa ujumla.

Akihutubia watanzania na wakazi wa afrika mashariki Rais Ndayishimiye amebainisha kuwa Tanzania imekuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi ya Burundi na nyingine

Ndayishimiye amesisitiza kuwa pamoja na kuwa Jirani wa nchi nyingi watu wake wana unasaba na nchi za Burundi, Kenya Uganda, Comoro, Zambia, Malawi na Zimbabwe na kusisitiza kuwa husezi kuwatofautisha kwa namna yoyote ikiwemo lugha na mahusiano ya kiutamaduni

Kwa upende wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan amehimiza watanzania kudumisha umoja wao ambao unaunganishwa na lugha ya Kiswahili sambamba na kuendeleza shughuli za maendeleo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesherehekea miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa na Marais wa kwanza wa nchi hizo hayati Julius Nyerere na Abeid Amani Karume

 

 

Post a Comment

0 Comments