Mbunge Byabato atoa heko kwa Dr. Samia, 15 Bil zaleta tija Bukoba

Zaidi ya shilingi Bilioni 15 zimetolewa na serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika manispaa ya Bukoba mkoani Kager ana kuchangia ukuaji wa sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Hayo yamebainishwa jana na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Mhe. Adv Stephen Byabato wakati akihutubia mkutano wa hadhara na wananchi wa Jimbo la Bukoba mjini ambao umefanyika katika viwanja vya Soko kuu la Manispaa hiyo.

Mhe. Byabato amesema kuwa katika miaka 3 ya Rais Dr. Samia Suluhu Hassan ambayo inahitimishwa mwezi huu serikali ya awamu ya 6 imetoa fedha nyingi ambazo zilisaidia kuboresha mindomibinu ya elimu, Barabara, huduma za afya na Uchumi kwa wakazi wa Jimbo la Bukoba mjini

Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara wa mbunge Stephen Byabato mjini Bukoba

Amesema kuwa kupitia fedha hi
zo baadhi ya maeneo ambayo hayakuwa na shule yamepata huduma hiyo kwa kujengewa shule mpya za msingi na sekondari sambamba na kuanzisha huduma za Viwanda, Biashara na uwekezaji.

Miradi mingine ya mafanikio ni pamoja na uwekaji wa taa za Barabarani, Marekebisho katika Soko kuu, Usafishaji wa mto Kanoni, Ujenzi wa Hospitali ya wilaya iliyopo Nshambya pamoja na uunganishaji umeme kwa wananchi kupitia miradi inayotekelezwa na wakala wa umeme vijijini - REA.

Mhe. Byabato akiwa ndani ya gari jipya la wagonjwa lililopokelewa kwa ajili ya jimbo la Bukoba mjini Mkoani Kagera

Kufuatia kuwepo kwa mafanikio hayo sambamba na uwepo wa mahitaji mengine ya maendele, Mheshimiwa Byabato ametumia fursa hiyo kuwahimiza wananchi kuendelea kushirikiana na serikali katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa.

Pamoja na mambo mengine Mh. Byabato amejindua mashindano ya mpora wa miguu katika jimbo hilo kwa kukabidhi jezi, mipira pamoja na pesa tasilimu kiasi cha sh. 200,000 kwa kila kata kwa ajili ya maandalizi ya Jimbo Cup

Mbunge Byabato akikabidhi vifaa vya michezo kwa ajili ya maandalizi ya kombe la Jimbo la Bukoba mjini mkoani Kagera

Marchi 19 mwaka huu Rais Dr. Samia Suluhu Hassan atatimiza miaka mitatu tangu alipoapishwa kuwa Rais kufuatia kifo cha alitekuwa rais wa jamhuri ya Muungano Dr. John Pombe Magufuli

Mwandishi: Mariam Kagenda

Mhariri: Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments