Profesa Ndalichako akutanisha mabalozi 490 kuelekeza uchaguzi


Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini Prof. Joyce Ndalichako metoa ufadhili wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuwajengea uwezo mabalozi wa nyumba kumi wapatao 490 kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa

Akihutubia wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika jana katika ukumbu wa Chuo cha Ualimu Kasulu, Prof. Ndalichako amebainisha kuwa, ametoa ufadhili huo baada ya kupata na kusoma mwongozo wa Chama cha mapinduzi wa kuimaridha mashina kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025

Amebainisha kuwa viongozi wa mashina wamepewa kipaumbele katika mwongozo mpya wa Chama ili kuhakikisha muundo wa uongozi na usimamizi wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi unakuwa shirikishi.

Nilitembelea makao makuu ya chama na kukabidhiwa mwongozo huu unaoonesha wajibu wa viongozi wa shina katika uchaguzi na usimamizi wa shughuli za maendeleo, baada ya kuusoma nilibaini kuwa njia kuu ya kuwawezesha mabalozi kutekeleza wajibu wao huo ni kuwapa mafunzo, na ndiyo maana nimetoa ufadhili huu ili mjengewe uwezo kwa kujua wajibu wenu na pia mfahamu nini ni dira ya Chama kuelekea chaguzi zijazo” alisisitiza Prof. Ndalichako

Prof. Ndalichako akiteta jambo na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Kigoma Zaituni Buyogera, kulia ni Katibu tawala wa wilaya ya Kasulu, na mwenyekiti wa halmashauri ya Mji ndugu Noeli Hanura


Profesa Ndalichako amebainisha kuwa viongozi wa chama ngazi ya shin ani msingi imara wa kusimamia na kulinda miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali huku akimpongeza Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika ngazi za mitaa na vijiji ambako viongozi wa Shina wanatoka

Ametaja miradi ya mafanikio katika jimbo la Kasulu mjini kuwa ni Pamoja na ujenzi wa shule mpya za msingi na sekondari, zahanati na vituo vya afya na miradi ya kimkakati ikiwemo miundombinu, maji na umeme.

Nikitafakari nilipochaguliwa kuwa mbunge wa jimbo miaka takribani minne iliyopita hali ilivyokuwa na hatua tuliyofikia kwa sasa, sina budi kumshukuru mheshimiwa Rais Samia kwa kutoa mamilioni ya pesa katika jimbo hili, ninyi mabalozi ni mashuhuda, tumeupiga mwingi na harakati za kuleta maendeleo zaidi zinaendelea” alisisitiza Mh. Prof. Ndalichako huku akishangiliwa na viongozi hao

Pamoja na mambo mengine Profesha Ndalichako amegawa Bendera 550 za chama cha mapinduzi zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili kwa ajili ya mashina yote ndani ya jimbo hilo kwa lengo la kuonesha uhai wa chama katika ngazi za ubalozi.

Akihutubia katika uzinduzi wa mafunzo hayo katibu wa CCM mkoa wa Kigoma Bw. Mobutu Malima aliyekuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, amepongeza uamuzi wa mbunge wa Jimbo la Kasulu mjini Prof. Joyce Ndalichako wa kufadhili mafunzo kwa viongozi wa mashina akitaja kuwa chama msingi wake ni Shina.

Bw. Malima amekiri kuwa kitendo cha kuwakusanya mabalozi katika mafunzo hayo ni cha thamani kubwa na kinapaswa kupongezwa, huku akiwahimiza mabalozi kuutambua umhimu wao

Mabalozi ndio viongozi wakuu wa Chama ngazi ya shina, ndio wenye mamlaka kamili ya kusajili wanachama wapya na kusimamia mienendo ya wanachama, na endapo mwanachama anakiuka miiko a maadili ya chama mabalozi ndiyo wanaotambua na kumpa mwanya mwenyekiti wa CCM taifa kuchukua hatua, kwa maana hiyo viongozi wakuu wa chama ni wawili yaani mwenyekiti wa shinda na mwenyekiti wa taifa, lazima tuwaheshimu na tuwajengee uwezo ili watimize wajibu wao ipasavyo” Alisisitiza katibu wa CCM mkoa wa Kigoma Mobutu Malima

Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma Ndg. Mobutu Malima (kushoto) akipiga makofi kufurahia jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wenyeviti wa Mashina ya CCM maarufu kama mabalozi wa nyumba kumi.

Bw. Malima amewataka viongozi wote wa kuchaguliwa kuendelea kuwatambua viongozi wa shina na kuwapa ushirikiano ili kukijenga chama na kukipatia ushindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu

Profesa Ndalichako nakupongeza sana kwa namna unavyofanya kazi za kibunge na kuimarisha chama, hakika ningekuwa mpiga kura wa Jimbo hili ningekupigia kura, bahati mbaya mie si mpiga kura wako lakini ninaamini utashinda, na niseme tu kitendo hiki cha kuwakutanisha mabalozi umewachiongea na wabunge wengine, nitaandaa walaka kutoa maelekezo kila jimbo lifanye jambo kama hili” Aliweka bayana ndugu Malima.



Viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo wa mafunzo kwa mabalozi ni Pamoja na mwenyekiti cha CCM wilaya ya Kasulu Bw. Mbelwa Abdallah, mwenyekiti wa UWT mkoa wa Kigoma Bi. Zaitun Agripina Buyogera, katibu tawala wa wilaya ya Kasulu kwa niaba ya Mkuu wa wilaya, viongozi wa halmashauri ya mji wa Kasulu na wazee wastaafu ambao kila mmoja alipongeza uamuzi wa Profesa Ndalichako kuwakutanisha viongozi wa shin ana kuwajengea uwezo

Baadhi ya madiwani walioshiriki uzinduzi wa mafunzo ya mabalozi wa nyumba kumi mjini Kasulu, Katikati ni Prof. Joyce Ndalichako

Hii ni Mara ya kwanza kwa viongozi wa CCM ngazi ya shinda kukutana kwa Pamoja katika ngazi ya jimbo tangu kuasisiwa kwa Chama cha mapunduzi mwaka 1977.


MATUKIO KATIKA PICHA

Profesa Joyce Ndalichako (kulia) akionesha msisimko wa kipekee wakati akishuhudia shamrashamra za mabalozi waliokuwa ukumbini tayari kupokea maelekezo ya Chama. Kushoto ni katibu wa CCM mkoa wa Kigoma Ndugu Mobutu Malima

Katibu tawala wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtewele akiwa na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Kigoma Bi. Agripina Zaituni Buyogera baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa mafunzo kwa mabalozi mjini Kasulu

Katibu wa CCM Mkoa wa Kigoma Ndugu Mobutu Malima (kulia) akiwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kasulu Ndg. Mbelwa Abdallah wakifuatilia maelezo kuhusu mafunzo kwa viongozi wa mashina ya CCM kuelekea Uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu

Katibu Tawala wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtewele (mwenye nguo yenye picha ya Rais Samia) mwenyekiti wa UWT mkoa wa Kigoma Bi. Buyogera (mwenye Kilemba) na Prof. Joyce Ndalichako wakipiga makofi kuashiria kufurahishwa na jambo ndani ya mkutano huo, Kulia ni Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa kasulu ndg. Noeli Hanura akipokea ujumbe wa maandishi katika simu yake

Baadhi ya Mabalozi kutoka kata ya Murusi Mjini Kasulu ambayo inaongozwa na Diwani wa CHADEMA wakifuatilia kwa umakini mwongozo wa viongozi wa mashina kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa 2024

  

Post a Comment

0 Comments