Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa
Halmashauri ya wilaya ya Kasulu Mh. Eliya Kagoma wakati wa kikao cha Baraza la madiwani
kilichofanyika leo katika makao makuu mapya ya halmashauri hiyo eneo la
Nyamyusi.
Mh. Kagoma amebainisha kuwa kikundi cha
Kamchape kimekuwa tishio la Amani kwa jamii wilayani humo na kimekuwa kikisababisha
uvunjifu wa Amani sambamba na uporaji wa mali za wananchi
“Licha ya kwamba Kamchape wamekuwa wakipora
mali za watu, wamesababisha chuki miongoni mwa jamii kutokana na kupandikiza
Imani za kishirikina na kusababisha jamii kutoaminiana” Anasema Mhe. Eliya
Kagoma
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kasulu
kanali Isack Mwakisu ametumia kikao hicho kuendelea kutoa wito kwa jamii
wilayani humo kukataa ushawishi wa kamchape na kutoa taarifa kwa vyombo vya
dola endapo watawabaini watu wanaijihusisha na kikundi hicho
DC Kasulu Kanali Isack Mwakisu apongezwa kwa kufanikisha udhibiti wa kikundi cha Kamchape ambacho kinahusishwa na uporaji na uchonganishi katika jamii mkoani Kigoma. Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu Mh. Eliya Kagoma pic.twitter.com/atMbfRYjL4
— BUHA FM RADIO (@FmBuha) May 9, 2024
Amewataka madiwani kutumia nafasi zao kutoa
elimu kwa jamii kuhusu kuepuka vitendo vya kishirikina vinavyochochea uvunjifu
wa Amani na kuzorotesha maendeleo
Vikundi vya watu wanaofahamika kwa jina la
rambaramba au kamchape vimekuwa tishio mkoani Kigoma kutokana na mwenendo wao
wa kuaminisha jami kuwa watu Fulani wanamiliki uchawi na kwamba wanao uwezo wa
kuondoa uchawi huo lakini wanapotekeleza kazi hiyo ufanya uhalifu ikiwemo wizi
na kuchochea chuki miongoni mwa jamii
Watu kadhaa wameripotiwa kupoteza maisha katika vurugu za kikundi cha kamchape huku makumi wengine wakikamatwa na jeshi la polisi kwa kusababisha uvunjifu wa Amani, uharibifu wa mali, uporaji na wizi.
Wakati huo huo mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu ametumia kikao cha madiwani kuwataka Viongozi wa kijamii, vyama vya siasa pamoja na madiwani kuepuka vitisho dhidi ya wananchi wanaoonesha nia ya kugombea uongozi wa serkali za mitaa utakaofanyika mwezi Oktoba 2024.
Mwandishi: Prosper Kwigize
Mhariri: Adela Madyane
0 Comments