Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) wapewa "HEKO"

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bi. Mary Maganga ameupongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa utoaji huduma unaofuata viwango vya Kimataifa katika kushughulikia masuala ya fidia kwa wafanyakazi. 


Mhe. Maganga amebainisha kuwa, WCF tayari huduma wanazotoa zimekidhi vigezo vya Shirika la Kimataifa la Viwango ikiwa ni, menejimenti ya vihatarishi, Huduma mtandao,Tathmini ya kisayansi ya Takwimu bima na Kanzidata, hivyo ameutaka mfuko huo kuhakikisha unakamilisha mchakato wa kuipata ithibati ya viwango vya kimataifa (ISO) ili kuendelea kutoa huduma bora na kuboresha utendaji.


Ameyasema hayo Mei 6, 2024 alipotembelea Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya ziara yaks ya kutembelea Taasisi zilizo chini ya Ofisi hiyo, ambapo amesema kuwa, Mfuko huo umekuwa ukitekeleza majukumu yake vizuri ikiwemo kulipa fidia kwa wafanyakazi walioumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi.


“Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni muhimu sana katika maeneo yetu ya kazi kwa sababu ni kiashiria kuwa serikali inatambua na kuthamini wafanyakazi nchini,” amesema


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mfuko huo, Dkt. John Mduma amemhakikishia Katibu Mkuu kuwa Mfuko huo utakamilisha mchakato wa kupata Ithiubati ya  ISO na ameongeza kuwa tayari wamepata Tuzo ya Kimataifa   kwa utoaji Huduma mtandao na Shirika la Kazi Duniani (ILO) limeutambua muongozo wa Mfuko huo inaoutumia kufanya Tathmini ya viwango vya Fidia.


Katika hatua nyingine Dkt. Mduma amesema, Tathmnini ya uhai na uendelevu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), iliyofanywa na Shirika la Kazi Duniani (ILO) inaonesha kwamba Mfuko una uhimilivu (Sustainability) kwa kipindi cha miaka 30 kuanzia mwaka wa tathmini 2022/2023.

Post a Comment

0 Comments