Sehemu ya bandari ya Kigoma katika Ziwa Tanganyika |
Mbunge wa Busega Mh. Simon Songe ametoa rai kwa wizara
yan uchukuzi pamoja na wizara ya fedha kurudisha mapato ya bandari kwa TPA ili
kuboresha na kuimalisha ubora wa Bandari nchini Tanzania.
Rai hiyo ameitoa leo wakati akichangia hoja ya bajeti
ya wizara ya uchukuzi katika Bunge la 12 linaloendelea jijini Dodoma
Amesema kumekuwa na changamoto nyingi zinazo
jitokekeza katika bandari baada ya mapato yanayo patikana kupitia TRA kutumika
katika sekta nyinginezo na kisha zinazo bakia kuwekwa katika mfuko.
Amebainisha baadhi ya changamoto wanazo kumbana nazo
ni kuchelewesha kulipa wakandarasi pamoja na kushindwa kukarabati miundo
mbinu kwa wakati
“TPA wanapata fedha kidogo na hazitoshi.” Amesisitiza
Simoni
Mh. Songe amehitimisha mchango wake kwenye bajeti ya
uchukuzi kwa kuiomba serikali kulipa fidia kwa wananchi wa Bariadi
Simiyu waliyo pisha ujenzi wa uwanja wa ndege
Amesema baadhi ya wananchi wanaishi maisha magumu na
wengine kuishi kama wakimbizi kwa kukosa maeneo maalumu ya kuishi kwa sababu ya
kucheleweshewa fidia zao.
Kwa upande wake mbunge wa viti maalumu CHADEMA Mh.
Ester Matiko ameiomba serikali kujenga uwanja wa ndege katika hifadhi ya Serengeti
ili kuondoa adha ya changamoto ya usafiri kutoka hifadhi moja hadi nyingine.
Amesema kumekuwa na changamoto kubwa wanayo kumbana
nayo watalii na wananchi wanapo toka mkoa mmoja kwenda mkoa wa Mara kulazimika
kutumia usafiri wa magari ambayo pia miundo mbinu yake sio rafiki.
Ameleza kuwa kumekuwa na miundo mbinu mibovu ya bara
bara inayo pelekea watalii wengi kutumia mda mrefu kwenda katika hifadhi ya
Serengeti pamoja na kutembelea katika kaburi la baba wa taifa hayati Mwalimu
Jullius Nyerere.
Mwandishi: Sara Mataro
Mhariri: Prosper Kwigize
0 Comments