RC Kigoma awapiga "mkwara" waajiri dhidi ya unyanyasaji

 

Mkuu wa mkoa Kigoma Mh Thobias Andengenye ameelekeza chama cha wafanyakazi mkoa TUCTA kuwachukulia hatua kali za kisheria waajiri watakao bainika kunyanyasa na kuwakandamiza watumishi wao.

Agizo hilo amelitowa  katika hotuba yake siku ya maadhimisho mei mos ambayo kimkoa yamefanyika  jana katika uwanja wa umoja wilayani Kasulu.

Amesema kuwa yapo malalamiko mengi kwa baadhi ya waajiri kuwakandamiza wafanyakazi wao katika mazingira ya kazi jambo ambalo ni kinyume cha sheria na pia ni utovu wa nizamu

Ameeleza kuwa ni vyema kwa mtumishi kutoa taarifa kwenye mamlaka husika kuhusu vitendo hivyo ili wamchukulie hatua za kisheria atakayebainika kukiuka kanuni za ajira

Sambamba na hilo amekemea vikali uzembe kazini pamoja wafanyakazi kuto toa ushirikiano mzuri kwa wananchi wanao tegemea huduma bora kutoka kwao.

Awali akisoma risala ya wafanyakazi katibu wa shirikisho la vyama vya waanyakazi (TUCTA) mkoa wa Kigoma Bw. Jumanne Magulu amesema kuwa moja ya changamoto inayo wakabili waajiriwa wengi ni kukandamizwa wakati wa majukumu yao.

Amesema waajiriwa wengi wamekuwa wakinyanyaswa na kushindwa kutoa ushirikiano kwa mamlaka husika kwa kuhofia kusimamishwa au kufukuzwa kazi.

Baadhi ya watumishi walio hudhuria katika maadhimisho hayo ambao majina yao hawakupenda kutajwa wamekiri kuwepo kwa vitendo vya ukandamizaji na manyanyaso kutoka kwa waajiri

Wamesema watumishi wa kike ndio wanakabiliwa na changamoto nyingi hususani unyanyasaji wa kingono.

Bi. Rose Marry Castor ambaye ni mkazi wa Heru juu na mjasiriamali akizungumza na Buha News amelalamikia kuwepo kwa uzembe miongoni mwa wafanyakazi wa taasisisi za Umma na ameomba watumishi kutambua majukumu yao wawapo kazini na kufanya kazi kwa kujali misingi ya taaluma zao.

Amesema baadhi ya watumishi wamekuwa wakitanguliza rushwa kwanza ndipo watoe huduma kwa wakati jambo ambalo kwa wanyonge na wasio jiweza hushindwa kupata huduma.

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 2024 imekuwa na kauli mbiu isemayo “Nyongeza ya Mashahara ni msingi wa mafao bora nak inga dhidi ya hali ngumu ya Maisha”

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments