Ruksa kuvuna mazao katika hifadhi za misitu maarufu Kagera Nkanda- Kasulu

Wizara ya Maliasili na Utalii imetoa maagizo kwa Wakala wa huduma za misitu Tanzania (TFS) kuwaruhusu wakulima waliolima katika hifadhi la pori la Kagera Nkana {Makere Kaskazini} wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma Kwenda kuvuna mazao yao kisha kusitisha kulima katika hifadhi.

Agizo hilo limetolewa Bungeni leo kufatia swali lililo ulizwa na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Kigoma Mh. Josephina Genzabuke akihoji nini tamko la serikali kuhusu wakulima walio zuiliwa na TFS kuvuna mazao yao katika pori la hifadhi la Kagera Nkanda.

Mh. Genzabuke amebainisha kuwa wakulima kutoka vijiji kurugongo, kaburanzwiri, Kagerankanda, Mvinza Nyakitonto, Mgombe, Nyachenda na Kitagata vya wilaya ya Kasulu wamezuiliwa kuvuna mazao yao hali inayohatarisha ustawi wa jamii hiyo.

Mh. Josephine Genzabuke Mbunge viti maalumu akiuliza swali Bungeni kuhusu wakulima kuzuiliwa kuvuna mazao katika hifadhi za misitu ya makere Kusini na makere Kaskazini wilayani Kasulu

Akitoa azimio la wizara ya Mali asili nan Utalii naibu Waziri wa mali asili na utalii Mh. Danstan Luka Kitandula ameagiza TFS kuruhusu kwa wakulima waliolima katika hifadhi za misitu wilayani Kasulu kuvuna na kisha wazuiliwe wasiendelee kulima katika misitu ya taifa.

“Tulishatoa maelekezo kwa wakala wa misitu Tanzania TFS kuwaruhusu wakulima hao kuvuna mazao yao na kisha wazuie asiwepo mkulima atakayeingia hifadhini kufanya shughuli hizo tena, sasa nitumie Bunge hili tukufu kuwaagiza TFS watoe kibali kwa wakulima wakavune nah atua zichukuliwe wasilime tena” amesisitiza Kitandula akizibu swali la nyongeza la mh. Genzabuke.

Hivi Karibuni diwani wa Kata ya Kurugongo Edson Hanyuma aliongoza wakulima zaidi ya 30 kwenda ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kasulu kuomba waruhusiwe kuondoa mazao yao katika mashamba waliyolima ndani ya misiti kufuatia TFS kupiga marufuku shughuli za uvunaji

Akiongea na buha News Mh. Hanyuma baada ya Bunge kuagiza wakulima kuruhusiwa ameipongeza serikali kwa kauli hiyo akitaja kuwa agizo limetoa faraja kwa wakulima wengi wilayani Kasulu.

Ameeleza kuwa tabia ya wakulima kuendelea kulima katika hifadhi hiyo kunatokana na kukosa maeneo maalumu ya kilimo na hivyo kujikuta katika mgogoro na TFS.

Amefafanua kuwa endapo serikali itatenga eneo maalum kwa ajili ya wakulima hao itasaidia kuondoa changamoto ya wakulima kuingia katika hifadhi.

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

 

Post a Comment

0 Comments