Sheria ya ndoa kufumulliwa kuzuia ndoa za utotoni

 


Serikali ya Tanzania imetangaza kukamilika kwa taratibu za uandaaji wa mswaada wa marekebisho ya sheria ya ndoa yam waka 1971 itakayozuia msichana kutoolewa kabla ya umri wa miaka 18 baada ya kukusanya ukusanyaji wa maoni na mapendekezo ya wananchi.

Hayo yemebainishwa leo na Naibu Waziri wa katiba na sheria Mh. Jumanne Sagini wakati akijibu swali lililo ulizwa na Mbunge wa viti maalumu Mh. Dr. Thea Medad Ntala akihoji lini serikali italeta mswada wa sheria ya ndoa ili kukabiliana ya ndoa za utotoni.

Mh. Jumanne Sagini amesema baada ya baada ya maamuzi ya Mahakama ya Tanzania, serikali iliwasilisha mswada wa marekebisho ya sheria ndogo kupitia tangazo namba moja la mwaka 2021 ilipendekeza umri wa ndoa kuwa miaka 18.

Amesisitiza kuwa Bunge kupitia kamati ya uongozi ilielekeza serikali kukusanya maoni ya wananchi kuhusu sheria hiyo na tayari hatua mbalimbali za ukusanyaji wa maoni zimetekeleza ikiwemo kufanyika kwa kongamano la sheria ya ndoa lililofanyika April 26 mjini Dodoma.

Kwa upande wake Mhe. Ester Maleko Mbunge wa viti maalumu akiuliza swali la nyongeza amehoji kuhusu lini serikali itafanya marekebiso ya sheria ya ndoa kipengeze cha utatuzi wa migogoro ya ndoa na matunzo kwa Watoto

Serikali kwa upande wake imebainisha kuwa yameshaundwa mabaraza ya usuluhishi ambapo moja ya kazi zake ni kutatuza migogoro ikiwemo matunzo ya watoto.

Naibu Waziri wa katiba na sheria Mh. Jumanne Sagini amekiri kuwa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kuhusu migogoro na fidia za matunzo ya watoto ina mapungufu kadhaa hasa kwenye viwango na anatoa maagizo kwa tume ya kurekebisha sheria katika maboresho yanayoendelea wazingatie pia suala la viwango vya fidia hizo

Aidha ametoa wito kwa wananchi ambao wataona au kukabiliwa na changamoto katika utekelezaji wa sheria hiyo wende mahakamani kudai haki zaidi.

Mwandishi: Sara Mataro

Mhariri: Prosper Kwigize

 

 

                                     

 

Post a Comment

0 Comments