Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.
Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi
walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-
i.
Amemteua Dkt. Ashura Abdul
Katunzi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Kabla ya
uteuzi, Dkt. Katunzi alikuwa Afisa Udhibiti Ubora Mkuu,
Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Dkt. Katunzi anachukua nafasi ya Dkt.
Athuman Yusuf Ngenya ambaye amemaliza muda wake.
ii.
Amemteua Bw. Hassan Juma Mnyika kuwa Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo. Kabla ya uteuzi, Bw. Mnyika
alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais – Ikulu. Bw. Mnyika anachukua nafasi ya
Bw. Lain Ephraim Kamendu ambaye amestaafu.
iii.
Amemteua Bw. Addo Missama kuwa Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi. Kabla ya uteuzi, Bw. Missama
alikuwa Afisa Mwandamizi, Ofisi ya Rais – Ikulu. Bw. Missama anachukua nafasi
ya Bw. Joseph Constantine Mafuru ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Sharifa B. Nyanga
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
0 Comments