DC Kasulu ahimiza utunzaji wa vyanzo vya maji na usafi

 

Wananchi wa wilaya ya Kasulu mkoa wa Kigoma wametakiwa kulinda na kutunza vyanzo vya maji kwa kupanda miti lafiki  ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Agizo hilo limetolewa leo katika kata ya kumunyika na mkuu wa wilaya ya kasulu Kanali Issack Antony Mwakisu wakati akizindua mradi wa maji uliowezeshwa na shilika la Hope Foundation katika mtaa wa Sunzu na Nyerere

Kanali Mwakisu amesema kila mwananchi anao wajibu wa kulinda na kutunza chanzo cha maji  sambamba na kuacha  kufanya shughuli za kijamii karibu na vyanzo hivyo.

Amesisitiza kuwa maeneo yote yenye vyanzo vya maji yanapaswa kuachwa kwanumbali wa mita 60 na sheria kali itachukuliwa dhidi ya wananchi watakao kutwa wanafanya shughuli za ndani ya mita 60.

” Maji ni uhai tuyatunze yatutunze  kila mwananchi awe mlinzi wa mwenzake kuhakikisha vyanzo vya maji vinalindwa  hiki ni kipindi cha kiangazi tunapashwa kulinda vyanzo” amesema Mwakisu

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu (aliyevaa truck suit) akifuatana na Diwani wa Kata ya Kumnyika Mh. Jonas Selemani (anayeongea na simu) na viongozi wengine wa Halmashauri ya mji Kasulu kwenye tukio la kuzindua mradi wa maji na usafi wa mazingira.

Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika la Hope Foundation Bi. Evelin Amos  amesema taasisi yake imejikita katika kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.

Amesema mradi huo umegharimu zaidi ya Shilingi million 4 ambazo zimepunguza kero ya maji kwa jamii mjini katika kata ya Kumnyika

Awali, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya mji wa Kasulu amewataka wananchi kutunza mji wa kasulu kwa kufanya usafi katika mazingira ya nyumbani kwenye vyanzo vya maji na maeneo ya biashara ili kuweka mji wa kasulu katika hali ya usafi.

Amesema kuwa ili mji wa kasulu upendeze umapaswa kuwa safi mda wote hivyo kila mwananchi anawajibu wa kutunza mazingira

Uzinduzi wa mradi maji katika kata ya Kumnyika limeambatana na zoezi la usafi ambalo limeongozwa na mkuu wa wilaya Mh. Issack Mwakisu wakianzia mtaa wa highway hadi ofisi ya mamlaka ya mapato TRA wilayani Kasulu.

Mwandishi. Sara Mataro

Mhariri. Prosper Kwigize

Post a Comment

0 Comments