Wakati Tanzania ikiungana na mataifa yote duniani kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia, matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu mbalimbali wanafunzi wa vyuo vikuu na vyuo vya kati katika miji mikubwa wanatajwa kuwa katika hatari kubwa za kufanya au kufanyiwa ukatili kutokana na tamaa zinazowaingiza katika biashara za ngono.
Uchunguzi wa kikosi maalumu cha
waandishi wa Habari umebaini kuwa Biashara ya ukahaba ni moja ya biashara
zilizowahi kutokea katika miaka ya nyuma na zinaendelea kuwepo katika jamii na maisha
ya watu, huku ikitajwa kua moja kati ya kitega uchumi miongoni mwa wanawake waasio
na maadili.
Tanzania ni moja kati ya nchi
isiyoruhusu biashara hiyo ikiwa ni kinyume cha sheria zilizowekwa,huku adhabu
mbalimbali zikiwekwa kwa wahusika.
Licha ya Serikali kuweka sheria kali kudhibiti
vitendo vinavyokiuka maadili, biashara hiyo imekua ikiendelea, Jiji la Dar es Salaam
likitajwa kuongoza huku wanafunzi wa vyuo vikuu nchini wakitajwa kua wahusika
wa biashara hiyo.
Makala
hii ya kiuchunguzi, itaangazia namna gani wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali wanavyojihusisha
na biashara hiyo.
Ukahaba
miongoni mwa wanafunzi wa vyuo vikuu limekua tatizo linaloikumba Tanzania kwa
sasa, huku wanafunzi wengi wakijikuta kukabiliwa na tamaa na changamoto za
kifedha na baadhi yao wakigeukia ukahaba kama njia ya kujipatia kipato kwa haraka
na kukidhi mahitaji yao ya kila siku.
Hali hii
inaibua maswali mengi kuhusu sababu ya tatizo hilo, athari zake, na nini
kifanyike kukabiliana nalo.
Uchunguzi
uliofanywa na wanafunzi wa uandishi wa Habari kutoka shule kuu ya uandishi wa
Habari na mawasiliano kwa umma SJMC katika vyuo mbalimbali nchini umebaini
kuwepo kwa wanafunzi wanaojihusisha na biashara hiyo.
Aidha
uchunguzi umebaini maeneo wanayofanyia biashara yakiwemo Riverside,Kitambaa
cheupe, Dansa club, Juliana Liquid club, Ancle’s Mikocheni na Royal tour (Samora
),huku wanafunzi kuanzia miaka 20 na kuendelea wakihusika na biashara hiyo.
Ni
majira ya saa 10 jioni timu ya uchunguzi ya waandishi kutoka SJMC wanafika
katika maeneo ya sinza A na kuzungumza na moja ya mwanafunzi (kiume) ambaye
amekua mteja wa wanafunzi wa kike wanaofanya biashara hiyo.
Shesiki Gonga (si jina halisi) umri miaka 23 kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam mkazi wa Sinza A ambaye ni mpangaji katika nyumba maarufu ya mama T amesema amekua akishuhudia wanafunzi wengi kutoka chuo hicho wakifanya biashara hiyo katika maeneo mbalimbali tajwa naye akiwa mtumiaji "Mteja" mkubwa wa wasichana hao.
“Nimeanza
kutumia wadada wanaojiuza tangu mwaka wa pili chuoni wakati wa weekend mimi na
marafiki zangu tukawa tunatembelea maeneo mbalimbali ya club pamoja na disco
tukawa tunawaona tunazangumza nao
kuhusiana na maswala ya mapenzi wakawa wanakubali, mkikubaliana unamchukua” alisema
Gonga
Gonga anaweka bayana kuwa kuwa baadhi ya wasichana waosoma nae darasa moja hukimbia na kujificha
pindi wanapogundua ni yeye.
‘’Nimekua
niakikutana nao sana wanafunzi tunao soma nao, wamekua wakiona aibu na kukimbia
kujificha wanapojua ni mimi” amesema.
Baada ya
mahojiano na Gonga kukamilika ikalazimu timu ya waandishi kutembelea maeneo
tajwa ili kujionea kinachoendelea huko.
Ni muda
wa saa mbili na dakika 15 usiku, maeneo ya Sinza, clabu maarufu ya Kitambaa Cheupe, timu
ya waandishi inajionea kundi kubwa la wasichana wakicheza muziki na wengine
wakipata vinywaji, huku wengi wao wakivalia nguo za nusu utupu.
Waandishi
wakabahatika kufanya mazungumzo na moja ya kijana aliyekuwa katika eneo hilo (jina
limehifadhiwa) amesema ni ngumu kutambua yupi ni mwanafunzi na nani siyo
kulingana na matendo yanayofanyika pale.
“Hapa
wanakuja mabinti mbalimbali kama mnavyowaona inakua ngumu kuwatambua
wanafunzi,kwa sababu wote wanakunywa pombe,nguo walizovaa ndio hizo unazoziona
asilimia kubwa miili yao iko nje.” alisema
Aidha aliendelea
kwa kusema kua nje ya kupata burudani ya muziki na vinywaji kumekua na biashara
ya ukahaba nyuma ya pazia ikiendelea.
“Wengi wanafanya biashara hapa kwa kujificha na kuigiza kama ni wateja wa kawaida hali inayofanya siyo rahisi kugundulika na watu, lakini unapowasogelea na kuzungumza nao kibiashara hufunguka na kuweka wazi”. alisema
Waandishi
hawakuishia hapo, siku nyingine muda wa saa 12 jioni, inafika katika maeneo ya
chuo cha uhasibu (IFM), na kuzungumza na baadhi ya wanafunzi kutaka kujua
sababu na ukweli wa jambo hilo miongoni mwao.
Yunusi
mohamedi Issa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo hicho, shahada ya Science
and Economic Finance amesema Maisha yamekua magumu hivyo inawalazimu wasichana
hao kuingia katika biashara hiyo
"Ni kweli
wapo wanafunzi wanaofanya vitendo vya ukahaba tena wapo wengi sana, hasa
kipindi ambacho Boom linachelewa kutoka au linapokuwa limeisha kutokana na kuwa
wanafunzi wengi huwa na madeni wanayokopa wakati hawana pesa, hivyo pesa ya
Boom inapoingia yote inaishia kwenye madeni."
Yunus ameongeza kuwa baadhi ya wanafunzi hubaki chuoni
nyakati za usiku kwa kisingizio cha kufanya majadiliano kuhusu masomo, lakini
huishia kufuatwa na watu wenye magari na kwenda wanapokujua.
Pia ameongezea
kuwa wanafunzi wa chuo hicho wamekua wakifanya shughuri zao katika maeneo
mbalimbali yakiwemo Pweza beach,Resort,club na Masaai Kinondoni.
Aidha kwa upande wake amejitambulisha kwa jina
moja la “J” wa Chuo cha Usafirishaji amesema amekua na marafiki ambao wanajihusisha
na biashara hiyo.
“Marafiki
zangu hao wanaishi maneo ya kigamboni wengi wao wanafanya shughuli hiyo kukidhi
mahitaji yao kutokana na ugumu wa Maisha wanayoishi wamekua na madeni mengi” alisema
Timu ya
waandishi kutoka SJMC ikafunga safari mpaka kwenye moja ha hosteli ya nje
inayopatikana maeneo ya Mikocheni A wanayokaa wanafunzi wa vyuo mbalimbali kuzungumza
na mlinzi wa hosteli hiyo kujua muda wanaotoka na kuingia wanafunzi hao hasa
muda wa usiku na usafiri unaokuja kuwachukua.
‘’wasichana
wamekua na tabia ya kutoka usiku bila kuaga, hata pia hawatoi taarifa,kuanzia muda
wa saa tano ndo wanatoka saana wengi wao wakiondoka hurudi ahsubuhi na mapema
na wanaorudi hurudi kuanzia saa nane za usiku,aah hapo nje ya geti hua nasikia
saana milio ya pikipiki”, amesema Mzee Mussa mlinzi wa hosteli ya wanafunzi
inayopatikana Mikocheni.A
Kasheshe Kipanga (Jina
limefichwa) ni mlinzi katika hosteli zinazopatikana maeneo ya ubungo,
alipoulizwa kuhusiana na swala la kutoka kwa wanafunzi hususani majira ya usiku,
amesema
"Wanafunzi wengi wana kawaida hiyo ya
kutoka usiku japo siwezi kujua wanaenda wapi na kufanya nini ila walio wengi
wanapenda kwenda kwenye kumbi za starehe hasa siku ambazo wanakua hawana
vipindi "
Aliongezea
kwa kusema mara nyingi wanaondoka kwa usafiri wa bodaboda, bajaji na wengine
magari, maarufu kama Bolt.
Kufuatia
hali hiyo waandishi wakazungumza na madereva wa pikipiki almaarufu bodaboda na
bajaji walio karibu na maeneo a vyuo na hosteli kutaka kujua ni maeneo gani
hasa huwapeleka wanafunzi hao nyakati hizo za usiku.
Benjamini
Balainga ni dereva bodaboda kutoka Barakuda
amesema amewahi kuwapakia kuwapeleka maeneo mbalimbali nyakati hizo.
“Ninawabeba
ndio na mara nyingi nawapeleka Club mbalimbali zikiwemo Leaders club, pia na
hapo Sinza kama unaelekea Makumbusho, jina la hilo eneo silifahamu na nikuanzia
saa tatu usiku” amesema Benjamini.
Kwa
upande wake Emanueli Mwalongo dereva bajaji kutoka Ubungo amesema wateja wake
wakubwa ni wanawake hasa wakati wa usiku.
“Maeneo
ninayowapeleka ni Riverside, Landmark, Sinza King park lounge na BNB lodge na
mara nyingi wamekua wasichana wadogo nikikadiria umri wao ni kama miaka 20
hivi”. amesema Mwalongo
Aidha
Isihaka Omary dereva bodaboda kutoka Kariakoo amesema mara nyingi wamekua
wakitumia mfumo wa Bolt kuwapeleka maeneo mbalimbali
“Wakati
wa weekend, wanawake ndio nimekua nikibeba sana na kuwapeleka baa na wengine
wako mtandaoni “wanarikwestiwa” unaenda unawabeba unawapeleka wengi ni mabinti
kuanzia wa miaka ya 2000. amesema Omary.
Matumizi ya Madawa ya kulevya na ulevi wa kupindukia unatajwa kuwa ndiyo nyezo wanayotumia wasichana hao kuondoa aibu wakati wanapotekeleza jukumu hilo la kuuza miili yao kupitia vitendo vya ngono, huku baadhi ya wanaume hutumia njia hiyo kuwalewesha ili wawapate kiurahisi bila kulazimika kulipa pesa kwa ajili ya ngono.
Wengi wa wanafunzi wanatajwa kujihami na madhara ya kile wanachokiita ajali kazini hususani magonjwa ya ngono, na mimba, hivyo hulazimika kutumia madawa mbalimbali kuzuia uwezekano wa kupata mimba au magonjwa.
Timu ya
waandishi ikatembelea baadhi ya maduka dawa za binadamu yaliyo karibu na maeneo
ya chuo kutaka kujua wateja wakubwa maeneo hayo na dawa zipi hasa hununuliwa
kwa wingi
Muuzaji
wa duka la dawa lililopo maeneo ya ubungo njiapanda ya chuo jina (limehifadhiwa)
alipoulizwa kuhusiana na aina ya wateja anaowauzia dawa amesema
"wateja
wangu ni watu wa aina tofati kama unavyoona kwasababu dula liko maeneo ya
barabarani na sehemu yenye mzunguko mkubwa wa watu hivyo watu tofauti tofauti
huja kununua japo wengi ni wanafunzi wa chuo ambao zaidi wapo maeneo haya"
Aidha
alipoulizwa kuhusiana na dawa ambazo wateja wake ni wanafunzi wa chuo hususani
jinsia ya kike wanazokuja kununua amesema huwauzia dawa za kawaida ambazo yeye
kama mmiliki wa duka la dawa amehalalishwa kuuza, lakini aliongezea kwa kusema
lipo kundi kubwa linalokuja kutafuta dawa hatarishi kama dawa za utoaji mimba
na dawa za kuzuia mimba hususani P2, nk ambazo yeye haziuzi kutokana na kwamba
zilizo nyingi haziruhusiwi kisheria na ni hatarishi kwa afya ya binaadamu.
Februari 6, 2024, jijini Dar es Salaam Waziri wa Afya Mh. Waziri Ummy Mwalimu wakati akifungua mkutano wa siku Mbili wa mapitio ya kimkakati wa PEPFAR COP muhula wa 23 kwa lengo la kutathmini hatua iliyofikiwa kuhusu mwitikio wa VVU katika kufikia udhibiti wa UKIMWI ifikapo mwaka 2030 alihimiza jamii kuzingatia kanuni za afya na kuepuka kuingia katika vitendo hatarishi.
“Hata
hivyo tunatambua kwamba kuna misuse ya hizi dawa hasa kwa watoto wa Shule ambao
kwa sasa inaonekana wanaogopa zaidi mimba kuliko UKIMWI! Matumizi holela ya P2
yanaweza kuzalisha matatizo mengine makubwa ya kiafya kwa wasichana/wanawake.
Wataalam wetu wamenihakikishia kuwa matumizi holela na ya mara kwa mara ya P2
yanaweza kusababisha ugumba na saratani.
Tunaendelea kuliangalia suala hili kwa mapana yake wakati tunaendelea kulijadili ndani ya Serikali na wadau, hatua ya haraka
tutakazo kuchukua ni kuongeza kasi ya utoaji elimu ya juu ya madhara ya
matumizi holela ya dawa hizi (P2). Nimeshawaelekeza timu yangu kulitekeleza
hili haraka.” amasema Waziri wa Afya Ummy
Mwalimu
Benedict
Nkwao ambaye ni Afisa Uhusiano Tasisi ya Ustawi wa Jamii alipoulizwa kuhusu
taarifa za biashara ya ukahaba miongoni mwa wanafunzi katika vyuo alisema hana cha kusema kwa sasa
kwa sababu hana Ushahidi kuhusiana na taarifa hizo na kusema masuala hayo
yanautaratibu wake pia katika kuyazungumzia
Katika
kuendelea kuzungumza na uongozi wa vyuo vingine hawakuonesha ushirikiano katika
jambo hilo.
Hivi
karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Amos Makala amebainisha mbinu iliyopo ya
kuondoa biashara hiyo katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo kutoa mitaji ya
biashara kwa wahusika ili wakidhi mahitaji yao na kuachana na biashara ya ngono.
“Kwa
hiyo tumeshaanza mikakati maalumu kuhakikisha angalau wengine tunawachukua wale
ambao wako tayari na kuwapa fedha kidogo ili wawe na mitaji yao binafsi” amesema
Albert Chalamila.
Moja ya hatari
zinazowakabiri wanawake na wasichana wanaofanya biashara za ngono ni uwezekano
mkubwa wa kupata magonjwa ikiwemo UKIMWI, kushambuliwa na makundi ya uhalifu,
kuingia katika uraibu wa madawa ya kulevya ikiwemo uvutaji wa bangi.
Pamoja na
athari za kisaikolojia wasichana wanaojihusisha na ukahaba wako katika hatari
kubwa ya kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja sambamba na kuingiliwa kinyume
na maumbile mambo ambayo yanadhalilisha utu na kuongeza maambukizi ya virusi
vya UKIMWI.
Wizara
ya Afya chini ya Waziri Ummy Mwalimu imeonesha takwimu ya maambukizi ya ukimwi
kupungua kutoka wa asilimia 7 mwaka 2003/2004 hadi kufikia asilimia 4.4 mwaka
2022/2023, kukiwa na tofauti kati ya watu na maeneo mbalimbali ya kijiografia.
Aidha, Waziri Ummy anasema kupaumbele katika masuala ya VVU/UKIMWI ni pamoja na kulinda mafanikio yaliyopatikana, kupunguza maambukizi mapya hususani kwa vijana walio katika umri wa balehe pamoja na kupunguza maambukizi mapya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
VIFUNGU VYA SHERIA.
Mahala pa kuhifadhi makahaba.
Sheria No. 49 ya 1962 s. 3 176A.
Mtu yeyote akiwa ni muuza kilabu ya pombe, hoteli, nyumba, duka, chumba au
mahali pengine panapofikiwa na watu mara kwa mara kwa ajili ya kununua au
kunywa viburudisho vya namna yoyote, anayeruhusu au kukubali kwa makusudi
makahaba wa kawaida kukusanyika na kubaki katika jengo lake kwa ajili ya
ukahaba, mtu huyo atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia atawajibika kwa
adhabu ya faini isiyozidi shilingi mia tano au, iwapo ni kosa la mara ya pili
na kuendelea atatozwa faini isiyozidi shilingi elfu moja
Wavivu na wazembe.
Sheria Nos 49 ya 1962; 11 ya
1983 Jedwal176 Mtu yeyote kati ya watu wafuatao:- (a) Malaya mzoefu
atakayefanya vitendo vya aibu mbele ya hadhara au kuzurura au kushawishi mahali
popote pa hadhara kwa ajili ya kufanya umalayaatahesabiwa kuwa ni mtu mvivu na
mzembe na atapaswa kulipwa faini isiyozidi shilingi mia tano au kifungo
kisichozidi miezi mitatu au vyote kwa pamoja.
KUHUSU KAULI YA MWANA SAIKOLOJIA
‘’Ni jambo ambalo linaweza
kumletea msongo wa Mawazo (anxiety) kwa kuhisi mambo mbali mbali ikiwemo
kuwa na wasi wasi labda kuhusu kutambuliwa na marafiki wake,familia au
hata wanafunzi wenzake chuoni, na vilevile pia kua na msongo wa Mawazo namna
ambavyo kama tunavyoona wanavyokatatwa na polisi na hata adhari za kiafya
kama magonjwa ya zinaa.
Na tunaona pia athari nyingine
kama Hatari ya Kukosa Mafanikio Kimasomo, wasiwasi, na matatizo mengine ya
kiakili yanaweza kuathiri utendaji wake darasani na kusababisha kushuka kwa
viwango vya masomo”. Amesema Mwanasaikologia Elias Lukata Kutoka tasisi ya
TUSPO
KUHUSU KAULI YA DAKTARI
“Kufanya ngono mara nyingi kwa
kipindi kifupi kunaweza kusababisha maumivu au uchungu kwenye maeneo ya siri
kutokana na msuguano na kuleta mchubuko jambo ambalo linaweza kuleta
adhari zaidi ya kupata magonjwa ya kuambukiza ikiwemo ukimwi,kisonono na
vilevile maambukizi ya bakteria kama vile vaginosis ya bakteria na maambukizi
ya fangasi, na hata hivyo Maambukizi ya mara kwa mara ya magonjwa ya zinaa
yanaweza kuathiri mfumo wa uzazi wa mwanamke na kusababisha matatizo ya kupata
mimba baadaye.”amesema dokta Mercy Mwanukuzi daktari kutoka hospitali ya
KAIRUKI.
TUKIO LA KUKAMATWA KWA MADADA
POA MAENEO YA SINZA.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hassan
Bomboko akiwa na Timu yake usiku wa June 15,2024 katika eneo la Sinza Jijini
Dar es salaam wameendelea na oparesheni ya kushtukiza kwa lengo la
kuyabaini na kuyafungia maeneo yanayotumiwa na Madada poa kuuza miili yao
(Madanguro) ambapo wamefanikisha kukamatwa Watu 30 wakiwemo Madada poa 25
pamoja na Wateja wao watano.
DC Bomboko amesema “Makaka poa na Madada poa, Mashoga na Wasagaji wote hawana
nafasi katika Wilaya ya Ubungo na wote wanaofanya biashara hizi warudi
wakafanye shughuli nyingine, naagiza hawa wote waende kituo cha Polisi na baada
ya Sikukuu wapelekwe Mahakamani na nielekeze oparesheni iwe endelevu maeneo
yote, Watendaji wa Mitaa na Kata, Maafisa Tarafa na Polisi Kata na wengine Mimi
nawaonesha mfano wajibu wa kupambana na Makahaba ni wa kwetu sote”
KAULI ZA VIONGOZI WA DINI
Imamu wa Masjid Nuru Mleni
Bakari Sarai amelizungumzia suala Hilo kuwa" Sheria ya kiislam inakataza
kuuza miili na ni zinaa inayofanyika, Mungu amesema ni njia chafu nakuhusu
watoto ni watoto hawana kosa ila watabaki watoto wamama kwasababu wamepatikana
katika taratibu isiyo ya kisheria "
Pia ameongezea kuwa suala Hilo
"Kiujumla nijambo lakulipiga vita mwisho litatuletea watoto mtaani"
Mchungaji wa kanisa la Grace
Primitive Baptist church Kenny John Mwankenja amesema"Biblia ndio kitabi
chenye utaratibu na kanuni kwenye agano la kale ilikuwa mtu akikamatwa anafanya
ukahaba au kuzini ni wanapigwa mpaka kufa Ukahaba hauruhusiwi sababu dini zipo
kusaidia kufuata taratibu Sheria na utamaduni, na ndoa za jinsia Moja
hazitambuliwi ila ndoa ya mke na mume ndo Biblia zinazozitambua kwa wazazi wa
pande zote mbili kulidhia na kanisa hutoa vyeti vya ndoa kwaniaba ya
Serikali na hakuna umri unaosema ndo unaruhusu kufanya biashara
hizo".amesema mchungaji Kenny
KAULI ZA WANAFUNZI WAOFANYA
BIASHARA CHUONI
Janeth John mwnafunzi wa
stashahada ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano Kwa Umma kutoka Shule Kuu ya
Uandishi wa Habari na mawasiliano kwa Umma ni mjasiliamali wa nguo za
ndani na kiume pamoja na Matisheti amesema “nashukuru mungu biasharaaa
inasaidiaaa ninapataa pesa ya kujikimu pia naepuka vishawishi na napenda
kuwashauri wanafunzi wenzangu wanao Fanya biashara ya kuuza Miili yao waaache
na kujiajiri wenyewe kwani biasharaaa inasaidiaaa sana”.
Mimi najishughulisha na biashara
ya perfumes,nimeamua kufanya biashara hii kutokana na kujipatia kipato
kulingana na maisha ya nyumbani kutokana mimi kama mtoto wakike kuna mahitaji
huwa na hitaji kupata kutokana na hayo mahitaji yangu nikaamua kuanzisha
biashara ili kuepusha vishawishi kutoka kwa wanaume na kutafuta pesa yangu
mwenyewe sababu hakuna vitu vya bure”amesema Sophia Daudi mwanafunzi
kutoka SJMC.
KAULI YA VIONGOZI KUTOKA CHUO
Dr Edga Ngelela mkuu wa kitengo
cha Mawasiliano ya Umma kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shule Kuu ya
Habari na Mawasiliano kwa Umma amesema
“kwanza nikianza
kuzungumza kihistoria suala kama hili la wanafunzi kujiuza limeanza tangu muda
na wakati Fulani tulikua tukisikia Sinza mara wapi kule na maeneo
mbalimbali maeneo ambayo watu hujiuza,sasa kwa kuanza kuzunguza sitaki
kuzungumza moja kwa moja kwa sababu ni mbaya kwa sababu kuna hali wanafunzi
akikusimulia unabaki kua dilemma,unakuta mwanafunzi ametoka kwao hana hela
amekuja kwenye hali ya kupata boom amepata asilimia 20 na hiyo asilimia 20 ana
wadogo zake wanasoma kwa hiyo ajigawie yeye wadogo zake na wazazi nyumbani
wanasema hela hakuna njia apekee anayogundua baadae kuifanya kwa sababu njia
zingine zoote za kufanya ilia pate pesa zimegoma kwa hiyo anamuua kuona njia
hiyo inamfaa,kwa maana nyingine amejitoa sadaka kwa familia yake,kwa hiyo ni
moja wapo ya hali inayoweza kupelekea mwanafunzi kuingia katika hali
hiyo”amesema Edga
Aidha ameongezea kwa kusema
masuala ya kuathiriwa kisaikologia kutokana na vitendo walivyofanyiwa ikiwemo
kubakwa na watuwao wa karibu imeka sababu ya wao kuathirika na kuendelea
kufanya vitendo hivyo.
“Imefikia hata wengine hatua ya
kutoweza hata kulala bila kulala na mwanaume kwa hiyo anaona njia nzuri ni
Kwenda kujiuza”
Pia Dr Edga amesema kuna kundi
lingine la wasichana ambao tamaa miongoni mwao imeka kishawishi kikubwa kwa wao
kujihusisha.
“kwamba Fulani ana kile na kile
unakuta nayeye anataka kua navyo kwa siku moja sasa hao nao wanaingia kwenye
shughuli hiyohiyo wanataka na wakati angeweza kufanya njia nyingine ya maana ya
kujikidhi”amesema Edga
Dr.Edga anaendelea kwa kutoa rai
kwa wazazi kucheza kwa nafasi yao katika malezi bora ya Watoto wao .
Aidha amesema kama chuo amekua
na kitengo maalumu cha kuwashauri wanafunzi ambao wamekua wakigungua wanapitia
adha hiyo kwa kuwapa ushauri na hata msaada wa kifedha.
“Lakini kumekua na watu wengine
wamekua na tabia tu ana kuona tu nisawa na kuona kumshauri ni kama umepitwa na
wakati,kwahiyo hata kumshauri inakua ni ngumu sana na huyu anaendelea na tabia
hizo.”amesema Edga.
KAULI YA MWENYKITI WA SERIKALI
YA WANAFUNZI DARUSO SJMC
“Ni kweli Kuna baadhi ya tetesi
zinazoonesha baadhi ya wanafunzi wanawake kujiuza, Mimi kama kiongzi kitendo
cha wanafunzi kujiuza ni mmomonyoko wa maadili kwasababu wote tumekua Kwa lengo
la kutafuta elimu na wazazi wetu wanatutegemea kwahiyo ukianza kujiingiza
katika biashara hiyo kunaweza kusababisha kwa mwanafunzi kushuka kitaaluma na
hata kupata magonjwa ambayo yatasabanisha kushindwa kufanya vizuri kitaaluma,
Kwahiyo ninaomba wanafunzi wenzangu kuacha hii tabia ili tuweze kutimiza lengo
la kuwa chuo na kuweza kuimarisha maisha yetu ya baadae kwaajili yetu na
familia yetu ya baadae pamoja na kuwasaidia wazazi wetu” amesema Ramadhani
Fupi.
KAULI YA MUHUSIKA
Anaitwa Loveness Chikawe
mwanafunzi wa mwaka wa tatu kozi ya Doctar of Medicine (MD) kutoka chuo
(kimehifadhiwa) amesema amekua akipitia changamoto nyingi hali iliyomlazimu
kujiingiza katika kitendo hicho.
“Mimi nyumbani ndio wa kwanza
kuzaliwa nimekua nikitegemewa nyumbani pia katika kuisaidia familia, nimeanza
shughuri hii tangu mwaka wa pili mwanzoni hivi baada ya kuona Maisha yanakua
magumu kwangu,boom ninalolipata limekua dogo kwangu halikidhi mahitaji yangu
kwa ujumla.”
Alipoulizwa ni kwanini
asingejikita katika biashara zingine kama wanafunzi wengine amesema”nilijaribu
nilivyoingia tangu mwaka wa kwanza nilikua nikiuza ubuyu ,pipi kwa wanafunzi
lakini bado haikuniletea faida kama nilivyotegemea kwa sababu hata Biashara
ikawa inatumia muda mrefu kuisha ikapelekea kushindwa kuendelea kuimudu”
Alipoulizwa biashara yake
huifanya vipi amesema “mimi tayari ninawateja zangu wenye mtandao kwa hiyo hua
ninatafutwa kwa njia ya simu tu, na hua ni watu wazima kuanzia kama miaka 45 na
kuendelea kwa sababu vijana wamekua na changamoto kubwa kwangu,unakuta
mnakubaliana hela Fulani lakini ukifika kule mkimaliza anakupa hela ambayo
hamjakubaliana lakini kwa watu wazima inakua ni tofauti kidogo.”
“Sijawahi kukutana na changamoto
yoyote kubwa ambayo labda ingenifanya niache,ninapata hela kama unavyoona
sasahivi niko kwenye chumba changu mwenyewe na kina kila kitu”amesema Loveness.
0 Comments