Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemtumia salamu
za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Hassan Babu kufuatia
kifo cha aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa huo Dkt. Tixon Nzunda kufuatia ajali
ya gari.
Kwa
mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, ajali hiyo iliyochukua
maisha ya Dkt Nzunda na dereva wake ilitokea majira ya saa nane mchana katika
eneo la njiapanda ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Wilaya
ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro alipokuwa kwenye ziara ya kikazi.
Rais
Samia anawapa pole ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu. Mwenyezi Mungu aziweke
roho za marehemu mahala pema peponi.
0 Comments