Tumieni likizo kulinda maandili na taaluma-Simbeye

 


Wazazi na walezi wa wanafunzi wa shule za msingi na sekodari wametakiwa kuwapa watoto  muda wa kutosha wa kujisomea badala ya kuwatuma kazi nyingi za nyumbani.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kasulu mkoani Kigoma Mwl Vumilia Julius Simbeye wakati akizungumza na waandishi wa habari 

Mkurugenzi huyo amesema  kuwa kila mzazi anao mchango mkubwa wa kupandisha kiwango cha ufaulu wa mtoto wake kwa kumtengea muda wakutosha wa kujifunza zaidi katika kipindi cha likizo.

“ Wazazi msitumie muda huu wa  likizo ya wanafunzi kuwapa kazi nyingi zitakazo wafanya washindwe kujisomea kwani tutakuwa tunatengeneza kizazi kisicho kuwa na elimu"

Vilevile mwalimu Simbeye ameeleza kuwa kipindi hiki cha likizo mzazi anapaswa kumlinda mtoto dhidi ya makundi  maovu yanayo lenga kudidimiza taaluma ya mtoto

Kwa upande wake mwalim wa shule ya msingi Nyarumanga iliyo katika kata ya Kigondo wilaya ya kasulu ambae hakutaka jina lake litajwe amekiri  kuwepo kwa ufauru hafifu wa wanafunzi kunakochangiwa na mwamko mdogo wa wazazi katika masuala ya kitaaluma

“tunapo funga muhula wa masomo na kuwapa watoto likizo  tuna maanisha kuwa mtoto anapo kuwa nyumbani akajiandae kisaikolojia kwa  muhula ujao ili kuongeza kiwango cha ufaulu  kwa kujisomea.” amesisitiza mwalimu huyo.

Imesisitizwa kuwa ni wajibu wa  wazazi kutambua nafasi yao katika taaluma ya mtoto hivyo mtoto apewe nafasi ya kujisomea na kufanya mazoezi ya kitaaluma ikiwa ni pamoja na kushiriki katika michezo ili kuimarisha afya ya mwili na akili wakati wa likizo

Mwandishi. Sara Mataro

Post a Comment

0 Comments