Mpya: Rais Samia apangua Mawaziri, TRA, ZRA zaguswa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-

 

   i.            Mhe. Dkt. Selemani Saidi Jafo (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Jafo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

 

ii.            Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Kijaji alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.

 

iii.            Mhandisi Yahya Ismail Samamba ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini. Kabla ya uteuzi huu, Mhandisi Samamba alikuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini. Mhandisi Samamba anachukua nafasi ya Bw. Kheri Abdul Mahimbali ambaye atapangiwa kazi nyingine.

 

iv.            Bw. Yusuph Juma Mwenda ameteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mwenda alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka  ya Mapato Zanzibar (ZRA).

 

 v.            Bw. Alphayo Japan Kidata ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais, Ofisi ya Rais - Ikulu. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Kidata alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

MAONI YA WANANCHI

Baadhi ya wananchi waliozungumza na Buha news kuhusu mabadiliko haya wametaja kuhusishwa na mgomo wa wafanyabiashara katika masoko mbalimbali waliokuwa wakishinikiza serikali kutazama upya mwenendo wa mamlaka ya mapato tanzania unaotajwa kuwakandamiza wafanyabiashara.

Mhe.Ashatu Kijaji aliyekuwa waziri wa Viwanda na Biashara na sasa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira

Imeelezwa kuwa Uhamisho wa Waziri wa Viwanda na Biashara Ashatu Kijaji na kamishna wa mamlaka ya Mapato tanzania TRA Bw. Alfayo Kidata ni sehemu ya usikivu wa rais katika kutekeleza maoni ya wafanyabiashara kuhusu mwenedo usiofaa wa mamlaka ya mapato na wizara husika.

Post a Comment

0 Comments