Dr. Mpango aitaka LATRA Kuwadhibiti madreva wa serikali

 


Na. Shukuruimana Revokatus

Makamu wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt.Philip Mpango awataka Mamlaka ya Usafiri Aridhini LATRA watoe elimu kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto.

Dkt. Mpango amesema hayo leo wakati wa kuzungukia mabanda yaliyojengwa katika uwanja wa jamhuri wakati wa maadhimisho ya uzinduzi wa  wiki ya nenda kwa usalama barabarani yanayofaniyika  kitaifa jijini Dodoma.

 Ameagiza Madereva wa magari, pikipiki Bajaji na vyombo vingine vya moto wapewe elimu ya kutosha kwa lengo la kuondoa kabisa ajari na vifo vinavyo sababishwa na ajari za barabarani nchini kote.

Dkt. Mpango amesema Madereva wanaoendesha gari za Serikali wanaendesha kwa kasi kubwa sana bila kujali foleni iliyopo barabarani hivyo LATRA wachukuwe hatua ya kisheria na  kutoa  mafunzo kwa madeleva hao ili wafuate sheria na kanuni za barabarani.

Ajali zimekuwa nyingi kwasababu ya madereva wanaoendesha vyombo vya moto kutopata elimu inayowaongoza ili kuokoa maisha ya watanzania dhidi ya vifo vinavyotokana na ajari za barabarani

Ameongeza kwa kuwapa pongezi Polisi wanao husika na usalama barabarani kwa kuhakikisha mifumo itakayo fanya kazi ili kusaidia kujua madereva wanaoendesha vyombo hivyo kwa kutofuata sheria za kitaifa.

Mkuu wa jeshi la polisi IGP Wambura anasema kutakuwapo na vifaa vinavyofanya ukaguzi wa magari hapa nchi ili kutokomea ajari za barabarani.

Mapambano dhidi ya ajari barabarani nila kutambuwa na nijukumu letu sote kwani kila mtu anao wajibu wa kutimiza.

Watu leo wamekusanyika na wadau mbalimbali wamekusanyika kwaajili ya kutoa nguvu na kutoa elimu juu ya matumuzi sahihi ya barabara kwa kuhakikisha ajari zinapunguwa na kuisha kabisa.

Jeshi lapolisi wanaendelea kufuata maelekezo ya Serikali kuhusu mifumo ya kielekituroniK ya udereva.

Post a Comment

0 Comments