Kasekenya atoa maagizo mazito kwa mkandarasi Simiyu


Naibu waziri wa ujenzi mhandisi Godfrey Kasekenya amemuagiza mkandarasi wa kampuni ya Rocktronic LTD anayejenga daraja la Itembe,Wilayani meatu mkoani Simiyu kukamilisha daraja hilo kabla ya msimu wa mvua kuanza .

Mhandisi Kasekenya  ametoa  maagizo hayo jana alipotembelea eneo la ujenzi wa  daraja hilo na kuridhishwa na mwenendo wa ujenzi unaofanywa na mkaandarasi mzawa.   

Jitahidi kuhakikisha ujenzi wa daraja hili unakamailika kwa wakati kabla ya msimu wa masika kuanza ili kuwe na uwezekano wa wananchi kupita katika daraja hili maana lisipokamilika tutakuwa tunarudi kulekule tulikotoka “

Mheshimiwa Kasekenya ametoa agizo hilo kufuatia jamii ya eneo hilo kulalamika kuwa wanaishi katika mazingira magumu kutokana na miundominu mibovu inayounganisha mkoa wa Arusha na Simiyu.

Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Geofrey Kasekenya akikagua ujenzi wa daraja. 
Picha na WJ Habari Simiyu

Gregory Msaki ni mkazi wa Arusha na John Joseph mkazi wa Bukundi  Wilayani  meatu wamesema kulikuwa na adha kubwa katika barabara hiyo na iliwalazimu kukaa siku 3  au zaidi bila kupita eneo hilo wakati wa msimu wa mvua jambo liloathiri maisha yao kijamii na kiuchumi.

Meneja wa Tanroads mkoa wa Simiyu Mhandisi Boniface Mkumbo akitoa taarifa ya ujenzi amesema daraja hilo lina urefu wa mita 150 na milango sita ya kupitisha  maji  na tayari ujenzi wake umefikia asilima 80.

Mkandarasi wa kampuni ya Rocktronic LTD David Sanagala amesema changamoto inayosababisha kuchelewa kwa ujenzi ni kutokana na kucheleweshwa kwa kwa malipo serikalini.

Sanagala anaeleza kuwa anadai zaidi ya shilingi bilioni 2 na ameiomba serikali kulipa fedha hizo ili waweze kuendana na kasi ya serikali .

Serikali inatekeleza ujenzi wa daraja hilo kwa gharama ya shilingi bilioni 8.4 na kukamilika kwake  kutarahisisha shughuli za kiuchaumi kwa mikoa ya Manyara, Simiyu, Arusha na Singida.

Mwandishi: Shukuruimana Revokatus 

Post a Comment

0 Comments