Dkt. Nchimbi awapongeza Rais Dkt. Samia na Prof. Ndalichako

 

Na. Shukuruimana Revokatus 

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Balozi Dkt. Emanuely Nchimbi amempongeza Mbunge wa jimbo la Kasulu Mjini Prof. Joyce Ndalichako kwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kutokana na fedha zinazotolewa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

 Balozi Nchimbi ametoa Pongezi hizo wakati akihutubia wananchi na wana CCM katika uwanja wa Uhuru Kiganamo mjini Kasulu akitaja kuwa Kasulu imebadilika hususani kwenye miondombinu na elimu na vituo vya afya.

‘’Kwa muda wa miaka mitatu maendeleo yamekuwa makubwa sana na tunatarajia baadhi ya miundombinu ambayo haijakamilika inakamilika haraka sana ili kuendelea na mambo mengine ya kuijenga nchi yetu” Amesisitiza Dkt Nchimbi

Katibu mkuu wa CCM ametumia pia fursa hiyo kueleza kushangazwa kwake na namna rais Samia Suluhu Hassan anavyoonesha uwezo mkubwa wa kuongoza taifa na kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli ya kisasa na bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere.

Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Emanuel Nchimbi akihutubia wananchi wa mjini Kasulu mapema leo ambapo pia amepokea kero za wananchi

Dkt. Nchimbi amebainisha kuwa baada kufariki kwa aliyekuwa mwasisi wa miradi mikubwa, jamii haikutarajia kuona rais mwanamke akiongoza vema utekelezaji na ukamilishaji wa miradi hiyo, lakini mama Samia ameonesha bila shaka kuwa wanawake wanaweza.

“Akina mama tembeeni kifua mbele, wanawake wanawaza na mama samia ameonesha mfano kuwa mwanamke anaweza kufanya mambo makubwa” amesisitiza Dkt Nchimbi

Awali, Naibu Waziri wa TAMISEMI Mh. Zainab Katimba alitumia mkutano huo kuonya wahudumu wa afya ya msingi kutotoza wananchi malipo ambayo hayajaidhinishwa na serikali akiwataka wananchi kutoa taarifa kwa viongozi endapo watapata usumbufu wowote.

“Nawaagiza wakurugenzi fuatilieni na hakikisheni huduma za afya ya msingi zinatolewa kwa jamii bila usumbufu wowote, na ninyi wananchi endapo mtakutana na vikwazo toeni taarifa kwa mamlaka husika ili matatizo yatatuliwe haraka.

Mh. Zainab Katimba naibu waziri wa TAMISEMI akihutubia wakazi wa mji wa Kasulu katika mkutano wa hadhara wa Katibu mkuu wa CCM.

Naye mmoja wa wananchi wilayani Kasulu Bi. Edina William amesema baadhi ya wahudumu wa vituo vya afya wamekuwa wakitoa tozo kubwa sana kwa wauguzi pa bila kufuata taratib za kituo husika na umekuwa niutaratibu ambao haujazoeleka ndani ya jamii

‘’Wahudumu wanaotoa huduma katika vituo vya afya waanapaswa kufuata sheria, kanuni  na taratibu za vituo husika, serikari imetoa maelekezo kulingana na umri wa mtu alio nao au rika tofauti kuhusu malipo yay a huduma za afya msingi.

‘’Mfano watoto kuanzia mwaka sifuri mpaka miaka mitano huduma zao ni bure lakini unakuta motto wa umri huo anatolewa malipo kitende ambacho siyo kizuri kabisa na mtu  kama ana bima ya afya isiwe sababu ya kumtoza pesa nyingine wakati amesha lipia’’ alisema William

Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi Dkt. Emanuel Nchimbi yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi na kusikiliza kero za wananchi.

Post a Comment

0 Comments