Sakata la ubakaji na ulawiti lamng'oa RPC Dodoma,


Mkuu wa jeshi la polisi  Nchini IGP Camillus Wambura amemuhamisha kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma  (SACP) Theopista Mallya  kwenda makao makuu ya polisi Dodoma na nafasi yake inachukuliwa na kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi (SACP) George Katabazi mbayae alikuwa kamanda wa polisi mkoa wa Manyara.

Mabadiliko hayo yanakuja baada ya  aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma kamishina msaidizi wa polisi SACP Theopista  Mallya kutoa taarifa yenye utata kwa vyombo vya habari  Agust 18 ,2024 kuhusu sakata la msichana aliyebakwa akitaja kuwa binti aliyebakwa na kulawitiwa  alikuwa anajiuza” 

Taarifa iliyotolewa mapema leo na msemaji mkuu wa Jeshi la Polisi David Misime mapema leo imesema, kauli iliyotolewa na aliyekuwa RPC Dodoma kamanda Mallya siyo msimamo wa Jeshi la Polisi

“Jeshi la polisi lingependa kutoa taarifa kwa kauli hiyo kama inavyoonekana kwenye kichwa cha habari siyo msimamo wa jeshi la polisi na kwamba kauli sahihi ya jeshi la polisi ni kama ilivyotolewa na msemaji wa jeshi la polisi kwa umma Agosti 4,6,9, 2024 “

Msemaji wa Polisi David Misime ameweka bayana kuwa watuhumiwa wa Kesi hiyo wanafikishwa mahakamani leo Agosti 19 jijini Dodoma .

Kabla ya  kuteuliwa kuwa kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma  machi  14, 2024 Kamshina msaidizi wa jeshi la polisi Theopista Mallya alikuwa kamanda wa mkoa  wa Songwe  na  nafasi yake kuchukuliwa na Augustino Senga ambaye alikuwa mkuu wa jeshi la polisi  Zanzibar

Kamanda  Mallya amedumu katika nafsi hiyo  kwa miezi mitano kabla ya kuondolewa mapema leo ambapo vyombo vya habari na wana harakati walifuatilia na kuandika kuhusu kauli yake yenye utata juu ya tukio la ubakaji.

Awali akifanya mahojiano na Gazeti la Mwananchi,Waziri wa maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi  maalumu Dkt. Dorothy Gwajima  aliwataka wananchi kuwa  watulivu kuhusu mwenendo wa upelelezi washitakiwa wa kesi hiyo akitaja kuwa haki itatendeka .

“Ndugu wananchi nimepokea hisia zenu ,maoni na maswali yenu ,amabayo mmeelekeza kwangu  nimewasiliana na mheshimiwa waziri wa mambo ya ndani tayari nae amepokea na anafanyia kazi hivyo tumpe nafasi atatoa taarifa yake"

Waziri Gwajima alisisitiza kuwa sheria itachua mkondo wake Nawasihi tujipe muda wa kuaamini kuwa haki itatendeka kwa mujibu wa sharia na itaonekana bayana na si vinginevyo

Video   ya tukio hilo la kikatili kwa binti  aliyedai ni mkazi wa Yombo Dovya jijini Dar es salaam ilianza kusambaa kwenye mitandao  ya kijamii Agosti 4, 2024, Ikimuonyesha binti huyo akibakwa na kuingiliwa kinyume na maumbile  na vijana 5 waliodai kutumwa na afande mmoja (hajatajwa) kufanya tukio hilo kutokana na kuwa na mahusiano na mume wake . 

Mwandishi: Hariath Kamgisha



Post a Comment

0 Comments