12 wahusishwa na Ujasusi nchini Iran


Serikali ya Iran imewakamata watu  12 wanaodaiwa  kuwa ni majasusi wa Israel,huku kikosi cha mapinduzi cha Iran kimesema watu hao walikuwa wanashirikiana na Israel kupanga njama ya kuvuruga usalama wa Iran.

Taarifa iliyotolewa na VOA Septemba 22,2024 kuwa kikosi hicho cha Iran kimebainisha kwamba majasusi hao 12 walikamatwa katika mikoa sita tofauti,nchini humo licha ya kutotaja siku waliyokamatwa.

"Wakati utawala wa Kizayuni na washirika wao wa nchi za Magharibi, hasa Marekani wameshindwa kufanikiwa katika mpango wao mabaya dhidi ya wananchi wa Gaza na Lebanon, hivi sasa wanataka kuhamisha mzozo nchini Iran kwa kupanga msururu wa njama dhidi ya usalama wa nchi yetu" taarifa ya kikosi hicho ilisema.

Septemba 19  mwaka huu Israel olitoa ripoti ya kumkamata  raia wake mmoja  kwa tuhuma za kuhusika katika njama na  Iran ya kumuua Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu na maafisa wengine wa idara za usalama za Israel 

Hata hivyo hali ya taharuki huko Mashariki ya Kati imeongezeka tangu kuanza kwa mgogoro kati ya Israel na kundi la wanamgambo wa Hamas huko Gaza, ambao ulitokana na kundi la Hamas kuishambulia kwa makombora Israel mwaka mmoja uliyopita na  Hivi sasa mgogoro  huo umeendelea mpaka nchini Lebanon na kundi la wanachama wa Hezbollah.

Mwandishi; Harieth Dominick

Mhariri; Sharifat Shinji

Post a Comment

0 Comments