Ajali ya Gari yakatisha Maisha ya Askofu Chediel Sendoro

Aliyekuwa Askofu wa Dayosisi ya Mwanga wa  kanisa  la  Kiinjili  la Kiluther Tanzania  (KKKT) Chediel  Elinaza Sendoro amefariki dunia usiku wa  jumatatu ya septemba 9,2024 kwa ajali ya gari iliyotokea Eneo la Kisangiro wilaya ya  Mwanga mkoani Kilimanjaro .

Taarifa iliyotolewa na  mkuu wa Kanisa la KKKT  askofu Dkt Alex Malasusa amesema ajali hiyo imehusisha gari la marehemu Askofo Sendoro ambalo liligongana na lori wakati askofu alipokuwa akielekea nyumbani kwake usiku .

Katika ajali hiyo marehemu alikuwa na mtoto wake ambae amenusurika na anaendelea na matibabu . 


Katika hatua nyjingine Rais  wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt: Samia Suluhu Hassan kupitia ukurasa wake wa Instagram  ametuma salamu za pole kwa  Mkuu wa Kanisa la  KKKT, baba askofu Dkt Alex Malasusa , Maaskofu wote ,waumini wote wa KKKT  , familia ,ndugu, jamaa na marafiki na kuwaombea faraja .

"Nawaombea faraja kwa neno kutoka katika Biblia takatifu kitabu cha Waebrania 13:14 "maana hapa hatuna mji udumuo bali twautafuta ule ujao mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi" 

 Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Simon Maigwa,akiongea na mwananchi  amesema ajali hiyo ilitokea 1:30 usiku siku septemba 9,2024 , Wakati gari lilokuwa likiendeshwa na Askofu huyo likitokea barababara ya Himo - Mwanga kuyapita magari mengine na kugongana uso kwa uso na Lori .

"Ni kweli leo saa 1: 30  imetokea ajali  na Askofu wa Sendoro amefariki dunia eneo la Kisangiro, Wilaya ya Mwanga , ambapo gari  aina ya Prado lililokuwa likiendeshwa na Askofu lilipata ajali na kusababisha kifo chake " alisema Kamanda "

Aidha Kamanda Maigwa amesema Chanzo cha ajali bado kinaendelea  kuchunguzwa na mwili wa marehemu tayari umechukuliwa kutoka eneo la tukio.  

Askofu Chediel Sendoro, ndiye askofu wa kwanza kuongoza Dayosisi ya Mwanga aliingizwa kazi Novemba 6,2016 baada ya  Dayosisi hiyo  mpya kuzaliwa kutokana na  kugawanywa kutoka dayosisi mama ya Pare . 

Mwandishi : Harieth Kamugisha  

Post a Comment

0 Comments