Bei ya Sukari Nchini Burundi Yapaa

 


Kiwanda cha sukari cha SOSUMO  nchini Burundi  kimetangaza ongezeko la bei ya sukari

 kutoka 3300  faranga ya Burundi hadi kufikia 8000 kwa kilo moja ya sukari ,bei   hiyo

 imetangazwa rasmi siku ya septemba  15 ,2024  na kiwanda hicho .


Akieleza sababu zilizopelekea kupanda kwa bei ya sukari Aloys

 Ndayikengurukiye Kiongozi wa kiwanda cha  sukari SOSUMO amesema kupanda kwa bei

 ya sukari kunatokana na changamoto ya upatikanaji  malighafi  pamoja na vifaa vya

  mitambo ya uendeshaji   kupanda bei katika soko la kimataifa. 


           Hii ni baadhi ya mifuko ya sukari inayozalishwa na kiwanda cha SOSUMO 

          kilichotangaza kupandisha bei ya Sukari nchini  Burundi  .


Katika hatua nyingine ,Wananchi wameonesha kusikitishwa na kupanda kwa bei ya sukari 

  wakisema kuwa imepandishwa zaidi  ya marambili ikilinanishwa na bei ya awali

 ,Ikizingatiwa na ugumu wa maisha  uliopo , hivyo  wameiomba serikali nchini humo

 kufanya tathimini ya bei hiyo  na kupunguza bei ya sukari . 


Hivi Karibuni Serikari ya Burundi ilikuwa imeruhusu wafanyabiashara kuingiza  sukari

 kutoka nje ya burundi,Kutokana na  kiwanda hicho kilichopo mkoani Rutana kusini mwa

 Burundi kutoweza kukidhi mahitaji ya sukari kwa raia wa Burundi.


Mwandishi: David Ndereyimana.

Post a Comment

0 Comments