Picha; DW
Rais wa Marekani Joe Biden septemba 17,2024 amezitolea wito pande zinazozozana nchini Sudan kushiriki tena kwenye mazungumzo ya amani.
Rais wa
Marekani Joe Biden ameziomba pande hizo zinazopigana nchini sudan kurejea kwenye
meza ya mazungumzo ili kumaliza tofauti zao na kurudisha vikosi vyao nyuma ili
kuwezesha misaada ya kibinadamu kuwafikia wahitaji bila vikwazo.
Aidha ameelezea
wasiwasi wake juu ya mji wa El-Fasher, moja ya miji mikuu mitano ya jimbo la
Darfur, ambao umezingirwa na wanamgambo wa RSF tangu mwezi Mei ambapo Mji huo
unakaliwa na wakazi karibu milioni 2 waliokimbia makazi yao
Vita vya Sudan
vilianza mwezi Aprili mwaka 2023 kati ya jeshi la Sudan na RSF, na tayari
vimesababisha vifo vya maelfu ya watu na wengine kuyakimbia makazi yao.
Mhariri; Eunice Jacob.
0 Comments