Bomu lapita na mguu wa Bobi Wine.

                                                                                      Picha: Abubaker Lubowa/ REUTERS

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda kupitia chama cha NUP Robert Kyagulanyi maarufu kama (Bobi Wine) amejeruhiwa mguuni  na bomu na kilipuzi chenye kutoa machozi wakati wa makabiliano na Jeshi la Police nchini humo.

Tukio hilo limetokea wakati kiongozi huyo alipokuwa njiani akisafiri kuonana na mawakili wake siku ya jumanne katika eneo la Buhindo takribani kilometa 20 kaskazini mwa mji mkuu wa nchini hiyo Kampala.

Jeshi la polisi nchini humo limetoa taarifa kuwa maafisa wa eneo hilo waliripoti kuwa kiongozi huyo alijijeruhi mwenyewe wakati akiingia kwenye gari lake.

Aidha kwa upande wa wataalamu wa afya katika hospitali ya Nsambya mjini Kampala wakati wakizungumza na waandishi wa habari wamesema kuwa wanatarajia kufanya matibabu ya upasuaji ya kuongdoa vipande vya bomu hilo.

Ikiripoti DW kuwa Bobi Wine atafanyiwa upasuaji, siku moja baada ya kujeruhiwa mguu katika tukio la vurugu ambapo chama chake jana kiliripoti kwamba alijeruhiwa kwa  Bomu la machozi.

Wakili wa mwanasiasa huyo, George Musisi amefahamisha kwamba hivi sasa hayuko katika hali mbaya ingawa kwa mujibu wa madaktari atafanyiwa upasuaji kuondowa vipande vya  bomu la kutowa machozi lililompiga mguuni.  

Imeandikwa na: Ramadhan Zaidy 


Post a Comment

0 Comments