CCM yalitetea jeshi la polisi tuhuma mauaji ya Kibao

Katibu mkuu CCM Dkt. Emmanuel Nchimbi.


Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Emmanuel Nchimbi  amesema haiwezekani kulihukumu jeshi la polisi kwa  baadhi  ya polisi wachache wanaofanya makosa kinyume cha sheria.

Dkt Nchimbi amsema hayo leo septembe 13,2024 wakati akitoa msimamo wa chama cha mapinduzi mbele ya  wahariri pamoja na waandishi wa habari waandamizi  katika ukumbi mdogo wa CCM, jijini  Dar es salaam, na kusisitiza kuwa  jeshi la polisi liko kwa ajili ya kulinda usalama wawanchi na mali zao.

Aidha Dkt .Emmanuel Nchimbi amsema Tangu mwaka 2017 hadi 2023 polisi 42 wameuawa na 141 wamejeruhiwa kutokana na kazi ya kuhakikisha  wanasimamia  usalama wa wananchi pamoja na malizao.

"Hatuwezi kulaumu jeshi zima la polisi kwa makosa ya polisi wachache hivi juzi kulikuwa na mtu alijifanya ni mwandishi wa habari aliyekuwa anapita katika taasisi za serikali akitaka pesa kwa madai ya kuandika makala za CCM  lakini nilipomuangalia usoni wala sio mwandishi wa habari ni tapeli,  sasa siwezi kuwalaumu waandishi wote wa habari  ni mtu mmoja"  amesema Dkt .Nchimbi.

 Katika hatua Nyingine Dkt . Nchimbi amesema ameamua kuzungumza na jamii  kutokana na hofu na sintofahamu  ya  utekaji na mauaji ya watu wasio na hatia  na kwamba CCM inalaani na haiungi mkono yanayoendelea nchini.

"Hakuna chama chochote dunia kinacho weza kuunga mkono wananchi wake kutekwa na kuuwa  kwasababu watakinyima kura kwahiyo tuache maneno ya uchochezi ,CCM hatuungi mkono viashiria vyovyote  vya uvunjifu wa amani"

Dkt Nchimbi ameongeza kuwa   viongozi wa chama  cha Dokrasia na maendeleo CHADEMA   Mbowe na Mnyika hawahusiki na utekaji na kuuwawa  aliyekuwa mjumbe wa sekretarieti  ya chama hicho badala yake uchunguzi ufanyike haraka ili kubaini wahusika  na wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria . 

Alipoulizwa na mwandishi wa habari ikiwa chama chake kitaruhusu wachunguzi kutoka nje ya nchi kuchunguza tukio la kifo cha Kibao  ,Dkt Nchimbi amesema  kuwa kazi ya uchunguzi ni wajibu wa serikali ila kama serikali itataka usaidizi kutoka nje, chama cha mapinduzi kikotayari kutoa ushirikiano. 

Katibu wa CCM  amesema hayo  wakati kukiwa na vuguvugu  la wananchi ,vyombo vyahabari na makundi ya haki za binadamu yakitaka serikali kufanya uchunguzi wa haraka ili kubaini waliyohusika na kifo cha Ali Kibao wa  CHADEMA.

Ali Mohamed Kibao alitekwa tarehe 6 septemba 2024 na watu wenye silaha   waliosadikiwa kuwa polisi, Eneo la kibo Coplex Tegeta jijini Dar es salaam  akiwa kwenye basi la Tashrif   akielekea nyumbani kwake Jijini Tanga na baada ya siku moja mwili wake ulikutwa  eneo la Ununio akiwa amepoteza maisha .

 Mwandishi: Harieth Kamugisha. 

Post a Comment

0 Comments