EU kuiadhibu Iran kwa kupeleka makombora Urusi

 

 Umoja wa ulaya (EU)  umetangaza kuchukua hatua kali dhidi ya Serikali ya Iran kutokana na uamuzi wake wa kuipatia Moscow makombora ya masafa marefu 

 Msemaji wa  EU Peter Stano amesema hayo usiku wa kuamkia September 10, 2024 , kuwa viongozi wa Brussels wanaendelea kuzifuatilia kwa kina taarifa hizo na iwapo zitathibitika watachukua uamuzi wa kuidhuru Iran juu ya uamuzi wao.

Hata hivyo  msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Iran, Nasser Kanani amekanusha vikali taarifa hizo na kudai kuwa  Iran haiwezi kuegemea upande mmoja wa vita vinavyo endelea kati ya Urusi na Ukreine .

Awali vyombo vya habari vya Marekani viliripoti  kuwa Marekani inaamini Iran inapeleka  silaha Urusi  za kutumia kwenye vita dhidi ya Ukraine.

 Kwa upande mwingine ,Msemaji wa Ikulu ya Kremlin, Urusi   Dmitry Peskov alikanusha  kuhusiana na  taarifa hizo na kusema si za kweli , wakati alipoulizwa na jarida la Wall Street nchini Marekani  .

 Iran na  Urusi wamekuwa washirika wa karibu katika nyanja mbalimbali ikiwemo ,kijeshi ,kibiashara na uchumi   tangu  wakati wa  vita  nchini  Syria .

Mwandishi: Ramadhani Zaidy

Post a Comment

0 Comments