Waziri Mavunde ametoa taarifa hiyo septemba 16,2024 katika hafla ya ufunguzi wa kikao kazi cha maofisa madini wakazi sambamba na maofisa kutoka Wizara ya Madini jijini Tanga na kuataka kuwa na mbinu thabiti ili kuweza kuzuia utoroshaji wa madini.
Aidha mavunde ameongeza kuwa watoroshaji hao wamekuwa wakitumia mashine za kuchakata mpunga ili kuweza kufanikisha zoezi la utoroshaji wa madini.
maofisa madini wakazi sambamba na maofisa kutoka Wizara ya Madini
Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni, kutoka tume ya madini ya serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imepata jumla ya shilingi trilioni 1.877 kutoka kwenye kampuni 44 zilizoshiriki katika sekta ya madini, mafuta, na gesi kwa mwaka wa fedha 2021/22 Kati ya kampuni hizo, 26 ni za madini, 7 ni za gesi asilia na mafuta, na 11 ni kampuni zinazotoa huduma katika sekta hizo.
Sekta ya madini inachangia zaidi ya asilimia 50 ya mauzo ya nje ya nchi, ambapo sehemu kubwa inatokana na dhahabu kwa mwaka 2022/2023 mchango wa sekta ya madini ni asilimia 9.6." Serikali kupitia sekta ya madini imeweza kukusanya shilingi bilioni 409.66 sawa na asilimia 85.43
Mwandishi; Jenipher Sanga.
0 Comments