Akizungumza Buha News ofisini kwake septemba 24 ameeleza kuwa idara yake imebaini hali hiyo baada ya kuendesha kampeni ya Mtu ni Afya iliyo anzishwa agost 1,2024 na kutembelea katika kata ya Muhunga na mitaa 06 na kubaini kuwa kati ya kaya 103 ni kaya 02 tu zenye choo bora.
Bw. Charles ameongeza kuwa ukosefu wa vyoo bora imekuwa ni changamoto kubwa katika mji huo hivyo inapelekea kuwepo kwa hatari ya kuzuka kwa magonjwa ya milipuko na kuongeza kuwa jamii inahitaji kupata elimu ili kuepuka magonjwa ya mlipuko.
Afisa Mtendaji wa mtaa wa Bwanyana Gaston Erasto ameeleza kuwa katika mtaa wake pamekuwa na changamoto ya vyoo kutitia hivyo kupelekea wakazi wa mtaa huo kuogopa kujenga vyoo kwa kuhofia hasara.
Kampeni hiyo yenye kauli mbiu isemayo fanya kweli usibaki nyuma lengo likiwa ni kuhamasisha ujenzi wa vyoo bora na kuepuka magonjwa ya mlipuko.
Mwandishi; Ellukagha Kyusa
Mhariri; Eunice Jacob
0 Comments