Kibondo yaweka historia miradi 10 yapitiwa na Mwenge wa Uhuru.

Jumla ya miradi kumi yenye thamani ya Zaidi ya shilingi bilioni 4 imekaguliwa, kuwekewa mawe ya msingi na kuzinduliwa na mbio za mwenge wa uhuru katika wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma.

Akisoma taarifa ya miradi hiyo mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Agrey Magwaza amesema kuwa miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na miradi ya maji, afya, barabara na elimu.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Muhambwe Dr. Frolence Samizi amesema kuwa serikali inaendelea kufanya kazi kubwa ya kuboresha miundo mbinu na kukuza uchumi hasa katika sekta ya elimu ambapo karibu kila kata ina shule ya  sekondari.

Aidha ameongezea kuwa kuwa katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita serikali imetoa Zaidi ya bilioni 58 kwa ajili ya kuboresha ujenzi wa miundo mbinu mbali mbali hali ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa kibondo kwa kiasi kikubwa.

Katika hatua nyingine kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ndg. Godfrey Eliakimu Mnzava amewataka viongozi katika wilaya ya Kibondo kusimamia vyema fedha zinazoletwa na serikali hasa katika sekta ya elimu, afya, maji na barabara ili kukuza uchumiwa nchi na jamii kwa ujumla.

Kwa muujibu wa taarifa iliyotolewa Septemba 14,2024 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma alipoupokea mwenge Mwenge huo wilayani Uvinza ukitokea mkoani Katavi alibainisha kuwa miradi (83) mkoani kigoma itapitiwa na mwenge wa uhuru huku ikiwa Jumla ya Miradi kumi(10) itawekewa Mawe ya Msingi, mitatu(3)  itafunguliwa, 27 itazinduliwa, 24 itatembelewa na kukaguliwa huku miradi 19 itahusisha ugawaji wa Vifaa kwa vijana wajasiriamali na misaada kwenye shule na vituo vya kulea watoto wenyemahitaji maalum.  

Mwandishi; James Jovin

Mhariri; Sharifat Shinji 


Post a Comment

0 Comments