Mwandishi wa habari Burundi atiwa mbaroni.




Mwandishi wa habari na kiongozi wa radio  Bw. Charles Makoto anashikiliwa na Jeshi la Polisi  nchini humo akishukiwa kupinga sheria (Rebellion).

Tukio hilo limetokea leo asubuhi tarehe 2 Septemba mwaka huu, ikitajwa kuwa Polisi zaidi 20 waliizunguka nyumba yake iliyopo Tarafa ya Mtimbuzi Jijini Bujumbura na kumtia mbaloni.

Hata hivyo sababu hasa za kukamatwa kwa Mwanahabari huyo bado hazijawekwa wazi na jeshi la Polisi la nchi hiyo huku wakiahidi kutoa taarifa zaidi  hapo baadae, ingawa taarifa zisizo rasmi zinasema amepinga sheria (Rebillion)


Charles Makoto ameingoza radio isanganiro kwa kipindi cha miaka 4, huku  Radio hiyo ikitajwa kuwa  miongoni mwa radio zinazosikilizwa zaidi nchini Burundi, pia ni miongoni mwa radio 3 zilizowahi kufungiwa kwa  miaka 5 zikishukiwa kupinga muhula wa 3 wa Hayati Rais  Pierre NKURUNZIZA.

Tarehe 14 August 2024  mwandishi na mtangazaji Floriane IRANGABIYE  BUHA  aliyekuwa ameshikiliwa  Gerezani  kwa kipindi cha miaka 2  nchini humo aliachiliwa huru baada ya mashirika ya haki za binadamu na waandishi wahabari kupinga unyanyasi huo 

Imeandikwa na : David NDEREYIMANA

Post a Comment

0 Comments