Kufungwa kwa ziwa Tanganyika kwa leta matokeo chanya kwa Wavuvi


             Mwananchi 

Mwenyekiti wa Wavuvi  Kibirizi Mkoani Kigoma Paul Samwel amesema hatua iliyo chukuliwa na Serikali kufunga Ziwa  Tanganyika imeweza kutoa matokeo chanya kwa wavuvi.

Mwenyekiti huyo amesema hayo septemba 12,2024 mkoani Kigoma baada ya mchakataji wa dagaa mwalo wa Katonga ziwa Tanganyika Zena Masoud kuchakata dagaa tani 1 baada ya ziwa kufunguliwa. 

Aidha bw. Paul Samwel ameongeza kuwa kwasasa wanachoendelea kupambana nacho ni kuboresha uhifadhi wa mazao  yanayo tokana na uvuvi na masoko ya   ndani na   nje ya  nchi  ili kuleta uchumi wenye tija.

Ziwa Tanganyika lilifungwa kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia Mei 15, 2024 na kufunguliwa August 16 na waziri wa mifugo na uvuvi Abdallah Hamis Ulega ,hali iliyorejesha  tena matumaini kwa wavuvi wa ziwa hilo .

Awali,mwaka 2023 kulikuwa na ukosefu wa dagaa na samaki kabla ya ziwa kufungwa, huku  upatikanaji wa samaki na dagaa  ukiwa  wa bei kubwa  kufikia  elfu 55  hadi  elfu 60  kwa kilo moja kutoka  elfu 10 ya mwanzo , ambapo kwa sasa zinapatikana kwa bei kati  ya elfu 20  hadi  elfu 22 .

 Mwandishi: Shukuruimana Revokatus

 

 

Post a Comment

0 Comments