Mabalozi wa EU Burundi na Tanzania watembelea wakimbizi Kigoma

 
Mabalozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania na Burundi leo anaungana na kutembelea kambi ya wakimbizi wa Burundi na DRC wanaoishi nchini Tanzania na kuzindua mradi wa pamoja unaovuka mpaka wenye lengo la kuwezesha wakimbizi kupata huduma hata wanaporejea nchini mwao.

Tukio hilo limefanyika leo katika kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma yenye zaidi ya wakimbizi wa Burundi pamoja na DRC

Akizungumza katika kikao cha pamoja cha wakimbizi, UNHCR, wadau na uongozi wa serikali ngazi ya mkoa na wizara za mambo ya nje na mambo ya ndani, Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania Bi. Christine Grau amesema Umoja wa Ulaya utaendelea kutoa misaada kwa wakimbizi na kwamba tayari imetenga kiasi cha Euro milioni 3 kwa ajili ya wakimbizi wa DRC waishio Nyarugusu huku akitangaza pia kuwa kiasi euro milioni 6 nyingine zimetengwa na umoja huo nchini Ubelgiji na zitatumika kutoa huduma kwa wakimbizi nchini Tanzania.

Kwa upande wake Balozi wa umoja wa Ulaya nchini Burundi Bi. Elizabetta Pietrobon ameeleza kuwa mradi uliozinduliwa ambao ulianza october 2023 una thamani ya Euro milioni 40 na inalenga kuwasaidia wakimbizi kupata huduma ndani ya kambi na baada ya kurejea ikiwemo kuwapatia vitambulisho vya uraia, vyeti vya kuzaliwa, elimu, na ndoa

Pamoja na ahadi hizo wakimbizi kutola Burundi na DRC hawajaonesha kuridhishwa na ahadi hizo huku wakisisitiza kuboreshwa kwa huduma ndani ya kambi na nchini Burundi, huku wakisisitiza kupewa fursa ya hifadhi nchi ya tatu

Picha ya pamoja ya mabalozi wa Umoja wa Ulaya Burundi Bi. Elizabetta Pietrobon na Balozi wa EU Tanzania Bi. Christine Grau (wa pli kushoto) pamoja na Kurugenzi wa idara ya wakimbizi Burundi Bw. Nestory Bimenyimana. Mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye, Bi. Birgite kutoka UNHCR Burundi, Sudi Mwakimbasi mkurugenzi wa wakimbizi Tanzania na mkuu wa wilaya ya Kasulu kanali Isack Mwakisu

Pamoja na madai hayo serikali ya Tanzania kupitia kwa mkurugenzi wa huduma za wakimbizi Bw. Sudi Mwakibasi pamoja na mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye wametoa wito kwa wakimbizi hususani wa Burundi kurejea na kwamba mradi wa Umoja wa Ulaya utakuwa na thamani rndani ya Burundi na si ukimbizini Tanzania

Mheshimiwa Andengenye amesisitiza kuwa ni wakati wa Wakimbizi hususani wa Burundii kuamua kurejea kwao kushiriki shughuli za maendeleoo na kusaidia Watoto wao kuishi na kuhudumiwa na taifa lao

Kikundi cha ngoma za asili kutoka DRC kikitumbuiza kuwalaki mabalozi na maafisa wengine kutoka UNHCR Tanzania na Burundi pamoja na viongozi wa serikali ya Tanzania katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma. Picha zote na. Prosper Kwigize

Wakati Tanzania ikihimiza wakimbizi wa Burundi kurejea, na wakimbizi wenyewe kulalamikia ualama nchini Burundi, Mkurugenzi wa idara ya wakimbizi nchini Burundi Bw. Nestory Bimenyimana ameeatoa hofu warudi kuwa Burundi kuna usalama wa kutosha na huduma za kijamii zimeimarishwa

Bw. Bimenyemina amebainisha kuwa kila mkimbizi anayerejea Burundi bila kujali umrii anapewa kiasi cha dola 220 zinazomwenesha kuanzisha Maisha mapya huku akisisitiza kuwa suala la usalama ni moja ya vipaumbele vya serikali Pamoja na wadau wakiwemo Umoja wa Ulaya na Umoja wa mataifa.

Baadhi ya mabweni ya pamoja kwa ajili ya waomba hifadhi kambini Nyarugusu

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Tanzania Kambi ya Nyarugusu ina jumla ya wakimbizi 135, 038 kati yao raia wa DRC ni 87,396 na Warundi ni 47,500 pamoja na waomba hifadhi kutoka Kenya, Uganda, Sudani Kusini, Somalia, Zimbabwe na Rwanda wapatao 142 ambao hawajakubaliwa kuwa wakimbizi nchini Tanzania

Post a Comment

0 Comments