Mahakama Kuu ya Masijala jijini Dar es Salaam imetupilia mbali ombi la Mbunge wa Kisesa Luhaga Mpina aliyeomba Mahakama hiyo imruhusu awasilishe majibu ya nyongeza katika kesi ya kikatiba dhidi ya Waziri wa Kilimo, Waziri wa Fedha pamoja na taasisi tano zikiwemo kampuni za vocha.
Mahakama imetoa uamuzi huo Septemba 18, 2024 kupitia kwa Jaji Arnold
Kirekiano aliyesikiliza shauri hilo baada ya kukubaliana na mapingamizi
yaliyowekwa na Serikali pamoja na wajibu maombi wengine walioomba Mahakama hiyo
isitoe nafasi na isikubaliane na maombi ya Mpina.
Aidha kwa upande wa jopo la mawakili wa Mpina wakiongozwa na Dk
Rugemereza Nshala ameomba mahakama iwape muda wa kupitia nyaraka za madai ya
kesi hiyo kisha kuwasilisha majibu ya nyongeza ili kesi hiyo itakapofika muda
wa kusikilizwa ushahidi uwe umekamilika.
Jaji Kirekiano amesema hawataruhusu watu wanaohitaji kuleta maombi mengine mahakamani hapo, kwa
ambao walikuwa wanaomba mahakama iwaruhusu wawasilishe majibu ya ziada baada ya
kupokea majibu kwa wajibu maombi.
Mpina amefungua shauri
hilo la kikatiba namba 18383/2024 akipinga mambo kadhaa ikiwemo uamuzi wa
Waziri wa Kilimo kutoa vibali vya ununuzi wa sukari kupitia Bodi ya Sukari kwa
kampuni ambazo hazimiliki viwanda vya sukari .
Awali kesi ya pili
ni Mpina dhidi ya Waziri wa Kilimo Waziri wa Fedha, Kamshina wa TRA na
Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na kampuni ya Itel na Zanzibar Merchandise
ambapo anahoji uhalali wa utaratibu uliotumika kutoa vibali vya uagizaji wa
Sukari ambapo Mpina anadai kuwa utaratibu huo ulikiuka Sheria, na kuwa vibali vinatakiwa kutolewa kwa muagizaji ambaye ni mzalishaji wa sukari.
Pia anapinga
Waziri wa Fedha kuruhusu Kamisha wa Mamlaka ya Mapato (TRA) kuamuru kampuni za
vocha kuingiza sukari nchini bila kulipa kodi na kupelekea Serikali kupoteza
mapato ya zaidi ya Sh1.548 bilioni pia amezishtaki kampuni za sukari kwa
kukubali kuingiza sukari na kupewa msamaha wa kodi.
Mwandishi : Shukuruimana
Revokatus
Mhariri:Abel Mahenge
0 Comments