Marekani yaondoa majeshi yake Niger

Marekani imesema kupitia Kamandi yake ya Uratibu Barani Afrika septemba 16,2024 imemaliza kuwaondoa wanajeshi wake nchini Niger na mchakato huo ulifanyika kwa awamu,  maamuzi hayo yanajiri baada ya serikali ya kijeshi ya Niger mnamo mwezi Aprili iliagiza Marekani kuondoa wanajeshi na watumishi wengine wapatao 1,000 nchini humo.

Kwa muongo mmoja uliopita, wanajeshi wa Marekani wametoa mafunzo kwa vikosi vya  Niger na kusaidia kukabiliana na ugaidi wa makundi ya Dola la Kiislamu na al Qaeda katika eneo hilo.

Awali,kabla ya mapinduzi nchi ya  Niger ilikuwa mshiriki mkubwa wa Marekani katika vita dhidi ya uasi katika ukanda wa Sahel, na kusababisha vifo vya maelfu na wengine mamilioni kuyakimbia makazi yao.

Washington inaangazia mpango mbadala katika eneo la Afrika Magharibi lakini mchakato huu unakwenda taratibu.

Tangu kupinduliwa kwa rais Mohamed Bazoum, utawala wa kijeshi,  chini ya uongozi  wa jenerali  Abdourahmane Tchiani,umekuwa na uhusiano baridi na nchi za magharibi, ikiwemo Mkoloni wake wa zamani  Ufaransa .

Mwandishi; Shukuruimana Revokatus

Post a Comment

0 Comments