Marekani na Uingereza zapinga Ukraine kutumia silaha za masafa marefu.

 

Rais wa marekani Joe Biden pamoja na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer wameahirisha maombi ya  Ukraine kutumia silaha za masafa marefu zinazotolewa na nchi za Magharibi katika vita dhidi ya Urusi.

Uamuzi huo umetolewa siku ya ijumaa ya September  13,2024 katika kikao kilichofanyika ikulu ya White House mijini Washington Marekani na kusema kulikuwa na majadiliano ya mda mrefu juu ya uamuzi huo.

Aidha waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer ameongeza kuwa nchi za Ulaya ya magharibi pamoja na Marekani  zipo kwenye  mkakati wa kutatua mzozo unaoendelea kati ya  Ukraine na Urusi.

Awali rais wa Urusi Vladimir Putin alitoa onyo juu ya mpango wa nchi za magharibi pamoja na marekani juu ya mpango wa matumizi ya silaha hizo na kusema kuwa hatua hiyo haiwezi kupunguza mzozo kati yake na Ukraine.

Katika juma liliopita rais wa Ukraine volodymyr Zelensky aliwasilisha maombi ya kutumia silaha za masafa marefu za Ulaya ya Magharibi pamoja na marekani kwa mara nyingine katika vita dhidi ya Urusi.

Mwandishi; Ramadhani Zaidy

 

Post a Comment

0 Comments