Mvua zasababisha mafuriko yalioua 30 Nigeria

         DW

 Mafuriko yaliyosababishwa na kuvunjika kwa kingo za  bwawa ,yamewaua  watu 30 na kuharibu makumi ya nyumba huko Maiduguri, mji mkuu wa jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria, 

Msemaji wa Wakala wa Kitaifa wa Usimamizi wa Matukio ya Dharura,bw. Ezekiel  Manzo amesema  kwamba idadi ya  watu waliofariki imefikia  30, na watu milioni moja wamepoteza makaazi yao.

 Kwa mujibu wa  taarifa iliyotolewa na shirika la umoja wa mataiafa la  kuhudumia wakimbizi (UNHCR)  nchini Nigeria  kupitia mtandao wake wa X imesema hayo ni mafuriko mabaya zaidi  kuwahi  kutokea nchini humo  katika kipindi cha miaka 30 .

Serikali ya jimbo hilo  imesema bwawa hilo lilivunjika kingo na kuhama mwelekeo wake   kutokana na mvua kubwa iliyonyesha  isivyokawaida.

 Mafuriko ya sasa yanakuja karibu miaka miwili, tangu mafuriko mabaya zaidi ya Nigeri yalioua watu zaid ya 600 kote nchini humo.

 

Mwandishi: Abel Mahenge.


Post a Comment

0 Comments