Mwenge wazindua nyumba ya watumishi Mwilamvya Mpya

Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru  kitaifa Ndg.Godfrey Eliakimu Mzava  amefanya uzinduzi wa nyumba ya watumishi  katika shule ya sekondari Mwilamvya mpya iliyopo wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma .

Uzinduzi huo umefanyika leo Septemba 18, 2024 katika shule hiyo huku kukiambatana na zoezi la upandaji miti na kusema nyumba hiyo itumike kwa matumizi ya walimu ambao hawana makazi  karibu na eneo la kazi. 

“ nyumba hii ianze kutumika mara moja  ili kupunguza kero za umbali na kuleta  thamani kwa Rais wa Jamhuri ya muungano  wa Tanzania Dkt. Samia maana hatuwezi kuzindua nyumba halafu isitumike, nyumba hii itumike kwa walimu waliopo au walimu wa ajira mpya” Amesema Mzava.

Aidha mwalimu Mkuu wa shule ya Sekondari Mwilamvya  Godwin  Baltazari ameshukuru na kusema kuwa ufunguzi wa nyumba hiyo  utawasaidia  walimu waliopo mbali na eneo la shule hivyo kutimiza majukumu yao kwa wakati  sahihi. 

“Uzinduzi huu utawasaidia walimu wanaoishi mbali  kutimiza majukumu yao kwa wakati maana walimu wakikaa mbali na shule wanashindwa kutimiza majukumu yao kwa wakati sahihi''Amesema mwalimu Godwin.

Mkimbiza Mwenge wa Uhuru akisoma maandishi ya jiwe la ufunguzi wa nyumba ya walimu katika shule ya sekondari Mwilamvya mpya, kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kasulu Prof. Joyce Ndalichako na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu

                        Zoezi la upandaji miti eneo la shule sekondari Mwilamvya mpya

Ifahamike kuwa Septemba 14,2024 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma aliupokea Mwenge huo wilayani Uvinza ukitokea mkoani Katavi ambapo kupitia taarifa aliyoitoa wakati wa mapokezi ya Mwenge huo,  Jumla ya Miradi kumi(10) imewekewa jiwe la msingi, mitatu(3)  itafunguliwa, 27 itazinduliwa, 24 itatembelewa na kukaguliwa huku miradi 19 itahusisha ugawaji wa Vifaa kwa vijana wajasiriamali na misaada kwenye shule na vituo vya kulea watoto wenyemahitaji maalum.

Mwandishi; Sharifat Shinji.

Mhariri: Ellukagha Kyusa.



Post a Comment

0 Comments